July 18, 2018


Real Madrid wamemweka mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard, 27 nambari moja kwenye orodha ya wachezaji inaowawinda kuchukua mahala pake Cristiano Ronaldo, ambaye amejiunga na Juventus. (Star)

Kipa wa Chelsea na Ubelgiji Thibaut Courtois, 26, anatarajiwa kujiunga na Real Madrid kwa payuni milioni 31. (Marca - in Spanish)

Ikiwa watamuuza Courtois, Chelsea watatathmini kumsaini kipa wa miaka 36 raia wa Czech Petr Cech kutoka Arsenal au kutoka Leicester raia wa Denmark Kasper Schmeichel, 31. (Sky Sports)

Nahodha wa Chelsea Gary Cahill, 32, anatathmini kukamilisha taaluma yake ya miaka sita huko Stamford Bridge mwisho mwa mwezi huu wakati klabu hiyo inafikia makubaliano ya paunia milioni 44.2 kwa mlinzi wa Jeventus na Italia Daniele Rugani. (London Evening Standard)

Chelsea bado wako mbioni kumsaini kipa wa Roma raia wa Brazil Alisson licha ya Liverpool kutoa ofa ya pauni milioni 62 kwa mchezaji huyo mwenye miaka 25. (Football Italia)

Aliyekuwa meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane, 46, atajiunga na Juventus, klabu ambayo raia huyo wa Ufaransa aliichezea kati ya mwaka 1996 na 2001 kama mshauri. (Libertad Digital)

Everton wako kwenye mazungumzo kumsaini wing'a wa Bordeauxraia na Brazil Malcolm, 21, kwa pauni milioni 30m. (Sky Sports)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic