SANCHEZ KUONDOKA MAN UNITED
Mshambulaiji Alexis Sanchez huenda akauzwa na Manchester United mwishpo wa msimu iwapo kiwango chake cha mchezo hakitaimarika , kulingana na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Ian Wright .
Sanchez, anayeripotiwa kupata mapato ya hadi £391,000 kwa wiki hajaonyesha kiwango cha mchezo wake kama alivyokuwa Arsenal kabla ya kujiunga na United mnamo mwezi Januari.
"Iwapo ningekuwa mfanyibiashara , ningetazama hali ilivyo halafu nianze kupanga ni wachezaji gani nitawauza'' , alisema Wright.
"Ni kwa sababu ya mshahara anaopata."
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 raia wa Chile alionyesha mchezo mzuri alipoingia United , katika mechi ya FA CUP dhidi ya Yeovil mwezi Januari, lakini hadi kufikia sasa amekuwa na mchanganyiko wa viwango vya mchezo wake akifunga mabao matatu pekee kati ya mechi 23.
0 COMMENTS:
Post a Comment