September 26, 2018


Mshambulaiji Alexis Sanchez huenda akauzwa na Manchester United mwishpo wa msimu iwapo kiwango chake cha mchezo hakitaimarika , kulingana na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Ian Wright .

Sanchez, anayeripotiwa kupata mapato ya hadi £391,000 kwa wiki hajaonyesha kiwango cha mchezo wake kama alivyokuwa Arsenal kabla ya kujiunga na United mnamo mwezi Januari.

"Iwapo ningekuwa mfanyibiashara , ningetazama hali ilivyo halafu nianze kupanga ni wachezaji gani nitawauza'' , alisema Wright.

"Ni kwa sababu ya mshahara anaopata."

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 raia wa Chile alionyesha mchezo mzuri alipoingia United , katika mechi ya FA CUP dhidi ya Yeovil mwezi Januari, lakini hadi kufikia sasa amekuwa na mchanganyiko wa viwango vya mchezo wake akifunga mabao matatu pekee kati ya mechi 23.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic