Bwire bado ana kumbukumbu za kufungwa bao 5-0 dhidi ya Simba katika mchezo wao uliochezwa jumapili amesema kuwa haikuwa mpango wa Mungu kuwapapasa Simba, hivyo wanakwenda kuwapapasa Mtibwa Sugar.
"Tupo vizuri, kikosi chetu ni cha ushindani morali ya wachezaji imeongezeka hivyo tunakwenda tukiwa tunajua tunataka kuchukua pointi tatu ugenini mbele ya Mtibwa.
"Tunauwezo wa kufanya makubwa, kufungwa haimaanishi hatuwezi, hivyo Mtibwa wajiandae kisaikolojia kupapaswa square maana hamna namna tumejipanga," alisema Bwire.
Mara ya mwisho Ruvu Shooting walipokutana na Mtibwa Sugar msimu uliopita kwenye Uwanja wa Manungu, Ruvu Shooting walishinda kwa mabao 2-1.








0 COMMENTS:
Post a Comment