MAFAILI YA WAARABU YAMFIKIA 'BOSS' SIMBA
Wakati Simba wakipambana na Waarabu JS Saoura, kesho Jumamosi tayari kocha mkuu wa timu hiyo, Patrick Aussems raia wa Ubelgiji amepeleka faili zima la Waarabu hao kwa ‘big boss’, Mohammed Dewji ‘Mo’.
Simba inatarajia kushuka dimbani kesho Jumamosi kuvaana na JS Saoura kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar ikiwa ni mchezo wa kwanza wa Hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo jumla ya timu 16 zinashiriki katika hatua hiyo.
Simba ipo Kundi D sambamba na timu za Al Ahly ya Misri na AS Vita ya DR Congo.
Taarifa ambazo Championi Ijumaa, imezipata kutoka Simba zinasema kuwa, katika ripoti hiyo ya Aussems aliyoikabidhi kwa Mo hivi karibuni ameweka mikakati yake kuelekea hatua ya makundi ikiwa ni pamoja na kuwaondoa Waarabu katika mchezo huo.
“Bodi ya Wakurugenzi ya Simba ilikutana hivi karibuni kujadili ripoti ya kocha kuhusiana na mechi za ligi na michuano ya kimataifa ambapo ripoti hiyo ilieleza juu ya mikakati yake ya kuifikisha Simba hatua ya makundi.
“Lengo kubwa ni kuhakikisha tunachukua pointi zote tisa za nyumbani kwa kuanza na mechi ya Jumamosi dhidi ya Waarabu JS Saoura ambapo tunahitaji kutua hatua ya makundi,” alisema mtoa taarifa huyo.
Simba imefanikiwa kutinga hatua ya makundi baada ya kuifunga Mbabane Swallows ya Eswatini kwa kuichapa jumla ya mabao 8-1 ikiwa ni pamoja na kuiondoa Nkana FC ya Zambia kwa mabao 4-3 hatua ambayo imewafurahisha viongozi hao.
0 COMMENTS:
Post a Comment