Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Snura alisema hakuwahi kupenda kutumwatumwa, alikuwa ni mvivu na kila alipoagizwa kufanya jambo alizua ugonjwa wa tumbo ili tu asifanye kazi husika.
"Uvivu huu acheni tu, sasa hivi nikikumbuka najiona mjinga, nilimsumbua sana bibi yangu kwa kusingizia ugonjwa, kila nikiona sasa natumwa nilikuwa naibua ugonjwa ambao sikuwa nao, bibi alinionea huruma na kunitungia jina flani kwani niliumwa kila siku," alisema Snura.
0 COMMENTS:
Post a Comment