Dakika 90 zimekamilika zinaongezwa dakika 4
FT: Mtibwa 1-0 Yanga
Uwanja wa Jamhuri Morogoro
Goooal Riphat Khamis dk ya 52.
Dakika ya 85 Yanga walifunga bao kupitia kwa Amiss Tambwe akimalizia pasi ya kichwa cha Ngasa ambalo mwamuzi alisema ni la kuotea.
Njano: Thaban Kamusoko kwa kosa la kumlalamikia mwamuzi akiwa nje ya uwanja.
Njano: Kelvin Kongwe wa Mtibwa Sugar dk ya 70 baada ya kumchezea rafu Abdalah Shaibu. dk ya 90 Salum Kihimbwa pia alionyeshwa kadi ya njano.
MCHEZO wa ligi kuu kati ya Mtibwa Sugar na Yanga unaochezwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro umekamilika.
Bao la Riphath Khamis wa Mtibwa Sugar a bao dakika ya 52 lililomshinda Kindoki liledumu mpaka mwisho wa mchezo wa leo.
Mashabiki wamejitokeza kwa wingi Uwanjani kuona namna ushindani ulivyo kwa timu hizi mbili hapa Morogoro.
REKEBISHA HEADING MKUUU MTIBW ANACHEZA NA YANGA SIO SIMBA
ReplyDeleteBLOG HAIKO MAKINI BADO
ReplyDeleteHawa waandishi lazima kucheki vyeti vyao,ni bomu kabisa
ReplyDeleteMakanjanja mnakimbilia wapi?
ReplyDeleteWanazi was Yanga hawa...wanapenda kuona Simba ikifungwa...ndiyo wanachotaka andika tu
ReplyDeleteAndikeni sasa jinsi Makambo anavyompoteza Kagere!Alipofunga mbili mlipata habari kuu ya kuandika
ReplyDeleteJee bado ubingwa wa Yangaaa?
ReplyDeleteZahera bado anaamini...ingawa bado kuna kazi ya kumfunga Azam mechi mbili au tatu kama watasonga mbele Azam FA cup
DeleteUsingizi mtamu sana leo. Zahera alifanya hesabu zake leo na akaona jinsi atavouteka ubingwa
ReplyDeleteYANGA..NINI ILE? TITANIC...YA!!
ReplyDeleteLABDA NOAH AJE!
Hongera sana mnyama kwa kufanya ulaluaji hapo Mkwakwani Tanga pia tuendelee kurudi nafasi yetu ya Ubingwa TPL.
ReplyDeleteKwa hiyo ndiyo Saleh Jembe hamandiki zaidi kuhusu matokeo ya mechi hizi zilizofanyika leo.Hebu rudini nyuma kwenye Siku Yanga inacheza na imefaulu...Muda kama huu tayari mlishatupia habari za mafanikio yao..Leo mmekosa LA kusema kwa sababu hesabu za ubingwa au mfungaji bora kotokea Yanga ni hazipo tens.Poleni Saleh Jembe na Yanga yenu
ReplyDeleteZahera hafai matokeo yanaonyesha kuwa wote Zahera na Mwandila na benchi lote la ufundi hawafai....Yanga wanacheza ovyo na matokeo ndiyo hayo yanaonekana...lazima jitihada zifanyike kunusuru hali hii
ReplyDeleteTFF na waamuzi pia mnajenga imani kwa watanzania kuwa mnawaonea Yanga kwa kukataa magoli yao....ligi ya mwaka huu tutajionea mengi....nadhani katika ligi zote hii ya mwaka huu imetia fora!...kwa madudu....Simba kucheza mechi 7 ndani ya siku 17...hata Patrick Aussems amelizungumzia hili...kwakweli tunapoelekea kama nchi si pazuri....si ajabu hata Serengeti Boys kutolewa....yaani laana inaitafuna TFF.....
ReplyDelete