May 14, 2019


KOCHA Mkuu wa Simba Mbelgiji, Patrick Aussems amesema kuwa mabao wanayoendelea kufunga washambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi na Mnyarwanda, Meddie Kagere ni sehemu ya ahadi waliyoitoa kwake baada ya kikao alichofanya nao.

Aussems amefurahishwa na safu hiyo ya ushambuliaji iliyocheza vizuri kwa kuelewana huku ikifuata maelekezo aliyowapa kabla ya mchezo.

“Nimewaambia wachezaji wangu wote wakiwemo washambuliaji akina Okwi, Kagere kuwa ninahitaji ushindi wa mabao mengi katika michezo iliyobaki ya ligi.

“Hivyo, ninafurahia kuona wachezaji wangu kadiri siku zinavyokwenda wanacheza kwa kubadilika wakifuata maelekezo yangu ninayowapa mazoezini nina matarajio makubwa ya kuwaona wakiendelea kubadilika kwa kufunga mabao mengi zaidi,”alisema Aussems ambaye bado Simba hawajampa mkataba mpya.

1 COMMENTS:

  1. kama wanabadilika kwa jinsi unavyowaelekeza maana yake tutegemee ukame zaidi, maana walifunga goli sita then umefuata ukame vs Kagera na Ukame vs Azam

    yupo kocha alituelekeza siri ya mfungaji ni UCHOYO, nina wasiwasi mwalimu amewaambia waache uchoyo ndio maana hawafungi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic