July 30, 2019

KIKOSI cha Azam FC kimeendelea na maandalizi ya kukata na shoka kwa ajili ya michuano ya kimataifa pamoja na Ligi Kuu Bara.

Azam FC ambao ni mabigwa wa Kombe la Shirikisho watapeperusha Bendera ya Taifa kwa kushirki michuano ya Kombe la Shirikisho.

Mchezo wao wa kwanza kimataifa unatarajiwa kuchezwa kati ya Agosti 10 nchini Ethiopia dhidi ya wapinzani wao Fasil Kenema.

Ofisa Habari wa Azam FC,Jaffary Maganga amesema kuwa maandalizi yapo sawa na wana imani ya kuleta ushindani.

"Kikosi kipo tayari kwa ajili ya michuano ya kimataifa, wachezaji wote wana morali ya kutosha na ni imani yetu kufanya vizuri, mashabiki watupe sapoti," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic