BAADA YA KUACHANA NA SIMBA, HUKU NDIPO ANAPOELEKEA NIYONZIMA
Imeelezwa kuwa nyota wa Simba, Haruna Niyonzima yupo kwenye mazungumzo ya mwisho na klabu ya AS Vita ya Congo na APR ya Rwanda.
Niyonzima amewaaga mashabiki wa Simba na kusema kuwa hivi karibuni atataja timu atakayoenda huku tetesi zikieleza kwamba ana nafasi kubwa ya kutua Congo.
Imeelezwa kuwa timu hiyo iliutambua uwezo wa Niyonzima baada ya kucheza na timu ya Simba kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mchezaji huyo ambaye aliwahi ia kuichezea Yanga alijiunga na Simba msimu wa 2016/17 baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika.
Inaonesha wazi kajiondoa mwenyewe shingo upande. Kama hunijui Mimi basi jaribu mwengine
ReplyDeleteHaloo nyie bana mnatuchanganya kabla ya kutoa taarifa muwe mnathibitisha kwanza. Mwanzoni mwa Wiki hii mlituandikia ameshasaini AS VITA kwa mil 80 leo mnatuambia yuko kwenye mazungumzo. Uzushi mtupu.
ReplyDeleteshule yao imeishia hapo, usiwalaumu
Delete