UONGOZI wa
KMC inayoshiriki michuano ya Kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho umeingia
mkataba wa miaka mitano na kampuni ya kubashiri ya M-bet wenye thamani ya
bilioni moja.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Meneja Masoko wa M-bet, Allen Mushi amesema kuwa wameamua
kuichagua KMC kati ya timu 20 ambazo zinashiriki Ligi Kuu Bara kutokana na
mafanikio ambayo wameyapata kwa muda mfupi.
“M-bet
tumeichagua KMC kutokana na namna ambavyo imejipambanua vema katika sekta ya
mpira baada ya kupanda daraja ilikuwa ikifanya vema na imeleta ushindani
mkubwa.
Mwenyekiti wa bodi ya
KMC, Benjamini Sitta amesema kuwa,: "M-bet
ni kampuni maalumu ya michezo ya kubashiri na tumeingia nao mkataba wa miaka
mitano wenye thamani ya bilioni moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment