PASCAL Wawa,
beki wa Simba amesema kuwa mashabiki wasiwe na presha kuelekea mchezo wa
marudiano wa kimataifa dhidi ya UD do Songo unaoatarajiwa kuchezwa kati ya
Agosti 23-25 uwanja wa Taifa.
Simba
inapeperusha Bendera ya Taifa kimataifa kwenye Ligi ya Mabingwa ambapo mchezo
wa kwanza wa awali wakiwa ugenini walilazimisha sare ya bila kufungana.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Wawa amesema kuwa mchezo wa marudio utakuwa mgumu ila
watapambana kupata matokeo chanya kwa kuwa watakuwa nyumbani.
“Mechi za
kimataifa zina ushindani wake na kila timu inahitaji kusonga mbele kwa sasa
tunajipanga kurudiana nao nyumbani imani yetu tutapata matokeo mazuri.
“Kwa sasa
hakuna haja ya kuwa na presha kubwa kwani makosa ambayo tuliyafanya mchezo wa
kwanza yamefanyiwa kazi na tunawaomba mashabiki watupe sapoti,” amesema.








Ohh vizuri sana tunapeta
ReplyDeletena hasa makosa ya defence line. hatutegemei kuona tunafungwa magoli ya free headers, clearances zinazorudisha mpira ndani ya box na overconfidence ya kupiga chenga ndani ya eneo la hatari. Bado mapema sana lakini tahadhari ni muhimu.
ReplyDelete