September 2, 2019



ETIENNE Ndayiragije, Kocha Mkuu wa Azam FC amesema kuwa kwa sasa anawapigia hesabu kali wapinzani wake wa kimataifa ambao ni timu ya Triangel FC kutoka Zimbabwe.

Triangel imepenya hatua ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kuiondosha Rukizno ya Burundi kwa jumla ya mabao 5-0 itamenyana na Azam FC iliyoiondosha Fasil Kenema ya Ethiopia kwa jumla ya mabao 3-2, kati ya Septemba 13 -15.

 Akizungumza na Saleh Jembe, Ndayiragije amesema kuwa tayari ameona makosa yao yalipo na ameanza kuwapa program maalumu vijana wake kwa ajili ya mchezo wake wa kimataifa.

“Nimegundu makosa ya vijana wangu yalipo na uwezo wao pia, taratibu ninakuwa na kikosi bora ambacho kitahimili mikikimikiki ya kimataifa nina imani ya kupata matokeo chanya.

“Kwa kuwa tutakuwa nyumbani ni wakati wa mashabiki kuendelea kutupa sapoti kama ambavyo walifanya awali kwenye mchezo wetu dhidi ya Fasil Kenema,” amesema Ndayiragije.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic