September 9, 2019



UONGOZI wa Mbeya City umesema kuwa umejipanga kufanya makubwa msimu huu kutokana na ushindani uliopo ndani ya ligi.

Mbeya City ilikuwa na mchezo Septemba 18 dhidi ya Yanga ambao umeondolewa na utapangiwa tarehe nyingine.

Sababu za kuuondoa mchezo huo umetajwa kuwa ni kuipa nafasi timu ya Yanga kujiaandaa na mchezo wa Klabu Bingwa Barani Afrika dhidi ya Zesco nchini Zambia.

Juma Mwambusi, Kocha Mkuu wa Mbeya City amesema kuwa timu ipo tayari kwa ajili ya ushindani wa ligi kuu msimu huu na itafanya maajabu.

Mchezo wa kwanza waliocheza Mbeya City ililazimisha sare dhidi ya Tanzania Prisons.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic