September 4, 2019



KOCHA Mkuu wa KMC, Jackson Mayanja amesema kuwa kwa sasa ameanza kuwapa mbinu mpya wachezaji wake ili kupata pointi kwenye mchezo wao wa ligi dhidi ya Coastal Union utakaochezwa Septemba 18.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mayanja amesema kuwa wametambua makosa yao kwenye mchezo uliopita dhidi ya Azam FC ambao walifungwa bao 1-0 wameanza kuyafanyia kazi.

“Kosa letu kwenye mchezo wa kwanza ilikuwa ni kushindwa kutumia akili kwa wachezaji wangu na kukosa umakini, tayari tumefanyia kazi makosa na tunaamini tutafanya vizuri.

“Michezo yetu yote iliyobaki tunahitaji kupata matokeo na hilo linawezekana kutokana na maandalizi ambayo tunayafanya,” alimema Mayanja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic