September 4, 2019


MAMBO yameanza sasa kwa timu ya Taifa kutafuta tiketi ya kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia ambalo litafanyika mwaka 2022 nchini Quatar kwa sasa ni muda wa kujiandaa kwa timu ambazo zitapata nafasi ya kushikriki michuano hiyo.

Hii ni michuano mikubwa namba moja duniani kote na yenye heshima kuliko mingine yoyote ambayo wacheza mpira huwa wanaifikiria na Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA) huitazama kiupekee katika maandalizi yake na ukamilishaji pia.

Muda huu ni muda wa kufanya kweli kwa timu yetu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kama ambavyo imeanza kwenye michuano ya Chan basi ni kuendeleza palepale ambapo iliishia kutoa burudani kwa mashabiki na Taifa kiujumla.

Wachezaji wote ambao wameteuliwa kuiunda timu ya Taifa wamepewa kazi ya kuwa mabalozi wa Taifa kiujumla watambue kwamba wanakwenda kufanya kweli na kuiwakilisha nchi kimataifa.

Thamani ya Bendera imejificha kwenye mioyo yao wasisasahau kwamba kuna Watanzania zaidi ya milioni 20 ambao wanawatazama kwa shauku na kuwaombea dua usiku hata mchana.

Ni leo Tanzania itakuwa inatupa kete yake ya kwanza kwa kucheza na Timu ya Taifa ya Burundi hapa sio pa kubeza hata kidogo kwa wachezaji pamoja na benchi la ufundi maana hawa ndugu zetu na majirani zetu wanatutambua vizuri nasi tunawatambua.

Hii inatokana na falsafa ya mpira wetu kuwakubli sana makocha na wachezaji kutoka nchini Burundi jambo ambalo linaleta picha kwamba wao wana kitu kama ambacho sisi tunacho ni jukumu letu kuonyesha utofauti ili kushinda.

Achana na suala la Kaimu Kocha kuwa raia wa Burundi hapa leo ni kazi tu kwani tayari mbinu za Burundi zipo mikononi mwetu basi wachezaji wasipuuzie hata kidogo mwenyewe amesema kuwa Burundi inabidi wamsamehe yupo kazini kazi iwe kazi kweli.

Mbinu zote ambazo wachezaji mnazo zinapaswa leo zitumike kwa ajili ya kuimaliza Burundi ndani ya uwanja bila kuhofia kwamba mpo ugenini na mwalimu ni raia wa Burundi matokeo kwanza mengine yatafuata.

Ikukumbukwe kuwa kwa kuanza kupata matokeo chanya mchezo wa kwanza kutafungua wepesi wa kazi na njia ya kusonga mbele kwani itakuwa rahisi kupata matokeo chanya nyumbani wakati wa mechi ya marudio.

Kwa kuwa tunaanza ugenini hilo halina shida wachezaji kazi yenu iwe moja kupambana kuzuia lango lisiguswe na mpira hata ule wa kuotea itasaidia kuwa na nguvu kwenye mchezo wenu wa marudio mtafanya vema na mtapata nafasi ya kusonga mbele.

Picha la kutisha inabidi lionyeshwe ugenini kwa kucheza kishujaa mwanzo mwisho mpira wa nidhamu na adabu kwa kuwa mpo ugenini mkitanguliza kiburi mtaumia mapema kabla mchezo haujaisha.

Makubaliano yenu wachezaji yawe kwenye kutafuta ushindi na kujituma mwanzo mwisho kwani Taifa linawategemea katika kuleta furaha siku ya leo kwenye michano mikubwa ambayo mnashiriki pambaneni bila kuchoka.

Taifa letu kwenye michezo hatua za kimataifa lipo chini sana hii inatokana na ubovu wa matokeo kwenye michuano mikubwa sasa kazi inaanza leo mbele ya Burundi tukipenya tu hapo tayari kuna pointi tutakuwa tumeongeza hapo itakuwa ni furaha kwa Taifa.

Ikishindikana kupata ushindi ngoma iwe sare tasa kisha kazi inakuja kumalizwa Taifa kishujaa kwa sapoti kubwa ya mashabiki mapema tu ushindi upo mikonni mwetu wenyewe inaitwa tushindwe wenyewe.

Kila la kheri wachezaji wetu tunaamini kwamba mpo sawa na mnatambua kuwa Taifa linawategemea tupo bega kwa bega nayi katika mchezo wenu mkubwa na mgumu kwani kila timu inatafuta matokeo nanyi mnapaswa mfanye kweli.

Hakuna kulala leo mpaka matokeo yapatikane ndani ya uwanja, chezeni kwa nidhamu itasaidia kupata ushindi mapema na kutumia uwezo wote ndani ya uwanja.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic