September 4, 2019


Na George Mganga

Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, amesema hakuna ukweli wowote juu ya kupewa mechi tatu na mabosi wake ambazo akipoteza atafukuzwa kazi.

Zahera amekanusha taarifa hizo wakati akizungumza na kituo cha Radio EFM jana jioni alipoalikwa  kutuoni hapo kwa ajili ya kuzungumzia mambo mbalimbali kuhusu timu yake.

Zahera ameeleza kuwa hajapewa mechi hizo na yanayoandikwa mitandaoni hayana ukweli wowote ule.

"Nani kanipa mechi tatu? Hakuna ukweli wowote kuhusiana na hilo.

"Kwani Barcelona hawajafungwa? Mimi nitaendelea kuwepo ndani ya Yanga, yanayoandikwa si ya kweli", alisema Zahera.


3 COMMENTS:

  1. Vita dhidi ya Yanga si ndogo....sasa tusubiri reaction ya wapenzi wa soka wa timu ya wananchi ....vurugu yake si haba ....itajengengeka dhana kuwa sheria na kanuni ziliundwa zikiwa na kusudio kwa mlengwa wa adhabu....Kuongoza Soka kwa chuki si "afya" kwa maendeleo ya mpira wa Tanzania....mapungufu ya kiutendaji na kiutawala yanapoainishwa na kusemwa inakuwa makosa....uhuru wa kukosoa na kutoa maoni ni uhuru wa kikatiba ambao kila mtu anao uhuru huu usikandamizwe kwa kutunga kanuni na sheria...ili kuzuia watu kukosoa mapungufu yanayotokea katika uendeshaji na usimamizi wa tasnia ya mchezo wa soka hapa Tanzania.

    USHAURI
    Yanga msitoke nje ya reli jiandaeni na Zesco mashabiki waujaze uwanja wa Taifa..ili muudhihirishie umma Yanga ni baba lao

    Ahsante

    ReplyDelete
    Replies
    1. Shida unaipenda yanga kuliko mpira...hoja dhaifu sn

      Delete
  2. Madhali anaogopwa atavuruga kila kitu

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic