October 11, 2019


Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) katika kikao chake cha Oktoba 7, 2019 ilipitia mwenendo na matukio mbalimbali ya Ligi na kufanya uamuzi ufuatao;

Viwanja: Kamati imezuia baadhi ya viwanja kutumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kutokana na kuwa na upungufu katika maeneo mbalimbali ikiwemo la kuchezea (pitch) na uzio wa ndani unaotenganisha wachezaji na washabiki (fence).

Viwanja hivyo ni Kinesi Bull (Dar es Salaam), Bandari (Dar es Salaam), Jamhuri (Morogoro), Namfua (Singida), na Mkwakwani (Tanga). 

Klabu ambazo timu zao zinatumia viwanja hivyo zimepewa nafasi ya kufanya marekebisho kipindi hiki ambacho Ligi zimepitisha mechi za kirafiki za FIFA au kuchagua viwanja mbadala vyenye sifa.

Vilevile klabu zimekumbushwa kuzingatia Kanuni ya 14(2), kwani baadhi yao zinapeleka viwanjani magari yenye kitanda badala ya gari la wagonjwa (ambulance). 

Kanuni imezungumzia ambulance, na si gari lolote tu.

Wasimamizi wa mechi vituoni wanatakiwa kuhakikisha ambulance zinapokuwepo viwanjani kama ilivyoelekezwa kikanuni. 

Kama huduma ya ambulance haitokuwepo wanatakiwa kuzuia mechi kuchezwa. Ligi Kuu ya Vodacom

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic