October 11, 2019


Mechi namba 19: Coastal Union 2 v KMC 0- Klabu ya KMC imetozwa faini ya sh. 1,000,000 (milioni moja) kutokana na timu yake kutoingia vyumbani wakati wa mapumziko katika mechi hiyo iliyochezwa Septemba 13, 2019 katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. 

Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi namba 24: Alliance FC 1 v Biashara United 1- Klabu ya Alliance imetozwa faini ya jumla ya sh. 1,000,000 (milioni moja) kutokana na vurugu za washabiki wake pamoja na kufanya vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina katika mechi hiyo iliyofanyika Septemba 20, 2019 Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.

Nayo klabu ya Biashara United imetozwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kufanya vitendo vinavyoashiria imani ya ushirikiana wakati ikiingia uwanjani. Adhabu zote ni kwa mujibu wa Kanuni ya 43(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Klabu.

Mechi namba 40: Kagera Sugar 0 v Simba 2- Mchezaji Zawadi Mauya wa Kagera Sugar amepewa Onyo kutokana na kitendo chake cha kumpiga mateke mchezaji wa Simba kwenye mechi hiyo iliyochezwa Septemba 26, 2019 katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. 

Adhabu dhidi yake ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Naye Mwamuzi wa mchezo huo Emmanuel Mwandembwa amepewa Onyo kwa kumuonesha Mauya kadi ya njano badala ya nyekundu kwa kitendo chake ambacho kilikuwa cha makusudi na kujirudia.

Mechi namba 41: Singida United 0 v Alliance FC 2- Klabu ya Alliance imetozwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kumweka kwenye benchi la ufundi Meneja ambaye hakutambulishwa katika kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting) wakati wa mechi hiyo iliyofanyika Septemba 28, 2019 Uwanja wa Namfua mjini Singida. 

Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi namba 44: Lipuli FC 2 v Tanzania Prisons 2- Klabu ya Tanzania Prisons imetozwa faini ya sh. 3,000,000 (milioni tatu) kutokana na basi lililobeba wachezaji wa timu hiyo kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi katika mechi hiyo iliyofanyika Septemba 29, 2019 Uwanja wa Samora mjini Iringa. Adhabu imezingatia Kanuni ya 14(49) kuhusu Taratibu za Mchezo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic