October 17, 2019


Tottenham huenda wakamtoa kiungo wa Mdenmark Christian Eriksen, mwenye umri wa miaka 27, na badala yake wakamchukua kiungo wa kati wa Real Madrid Muhispania Isco, mwenye umri wa miaka 27, katika kipindi cha uhamisho wachezaji mwezi Januari . (El Desmarque, via Express)

Arsenal wameripotiwa kutoa ofa kwa Real Madrid kwa ajili ya winga Muhispania Lucas Vazquez, mwenye umri wa miaka 28, kabla ya kipindi cha uhamisho cha Januari (El Desmarque, via Football.London)

Meneja wa zamani wa Juventus Massimiliano Allegri anaweza kumchukua mshambuliaji wa wa Croatia Mario Mandzukic, mwenye umri wa miaka 33, na kiundo wa kati wa Mjerumani Emre Can, mwenye umri wa miaka 25, pamoja nae katika Manchester United ikiwa atachukua nafasi ya Ole Gunnar Solskjaer kama meneja wa United. (Tuttosport, via Express)

Arsenal wameripotiwa kutoa ofa kwa Real Madrid kwa ajili ya winga Muhispania Lucas Vazquez,
Badala yake , Manchester United watasaini mkataba na wachezaji sita katika vipindi sita vya dirisha la uhamisho akiwemo Moussa Dembele kutoka Lyon, kiungo wa kati wa Atletico Madrid Saul Niguez na James Maddison Leicester City (Mail)

Anderlecht wamepigwa faini ya pauni ya £4,315 na shirikisho la soka la Ubelgiji kwa kumteua mlinzi wa zamani wa Manchester City Vincent Kompany, mwenye umri wa miaka 33, kama kocha mkuu wakati hana vigezo vya kufuzu . (Sun)

Mshambuliaji wa kati wa Manchester City Muargentina Aguero, mwenye umri wa miaka 31, amegongesha gari lake la Range Rover lenye thamani ya pauni £150,000 alipokuwa akielekea kwenye mazoezi lakini hakuumia . (Mail) Newcastle watatoa ofa ya miaka mitano zaidi ya mkataba na mchezaji wa safu ya mashambulizi Muingereza Matty Longstaff. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 19-anakamilisha mkataba wake msimu ujao. (mail)

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic