LICHA ya
timu ya Yanga kucheza jumla ya michezo mitatu ambayo ni sawa na dakika 270
imeipoteza Simba ambayo imecheza michezo minne ambayo ni sawa na dakika 360 kwa
kupata kona chache na kufunga bao.
Kwenye jumla
ya michezo mitatu iliyocheza mpaka sasa Yanga imepiga jumla ya kona 16 huku Simba
ikipiga jumla ya kona 17 na kwenye kona hizo Simba haijaambulia hata bao la
kuotea huku Yanga ikipata bao moja.
Simba
ilianza kupiga kona tano kwenye mchezo wake wa kwanza dhidi ya JKT Tanzania na
jukumu la kupiga mipira hiyo kuachiwa Clatous Chama, kisha ikapiga kona 6 dhidi
ya Mtibwa Sugar, kona 2 kwa Kagera Sugar na kona 4 mbele ya Biashara United
ikaambulia patupu.
Yanga
ilianza kupiga kona 9 dhidi ya Ruvu Shooting, ikapiga kona mbili mbele ya
Polisi Tanzania kabla ya kupiga kona 5 mbele ya Coastal Union ambapo walipata
bao la ushindi.
Kona hiyo
ilipigwa na Mrisho Ngasa uwanja wa Uhuru na ilipachikwa kimiani kwa kichwa na
kiungo Abdulaziz Makame na kuipa Yanga pointi tatu kwa mara ya kwanza baada ya
kupoteza mchezo wa kwanza mbele ya Ruvu Shooting na kulazimisha sare mbele ya
Polisi Tanzania uwanja wa Uhuru.
Yaan mm sion kama kna jambo la maana apa simba ina michezo 4 ina point 12 yanga michezo 3 ina point 4 nashangaa mwaandish wa hii blog unashangilia Kona walio funga
ReplyDeleteHu ni upuuzi. Simba mechi tatu points9 wakati Yanga mechi tatu points4? Sasa ukimuona mwanamme halisi anasherekea kukonyeza nakuwaacha watu wanaendelee kugonga basi ujue huyo mtu si mzima.
ReplyDeleteHuyu mwandishi huwa anawaza nini hivi dah blog ya hovyo hii
ReplyDeleteUgoro mtupu
ReplyDeleteSaleh Ally do something .Blog yako inapoteza weledi kwa kasi. Ujinga na kulinganisha mambo ya ajabu.
ReplyDeleteKuna mwandishi kanjanja ndio anaiharibu blogu.Uliona wapi watu wanalinganisha kona?Tunangoja mipira ya kutupa na faulo.Naacha rasmi kusoma hii blogu.
Hivi hawa TCRA hawaoni upuuzi wa hii blog?Wanatoza faini vituo na blog zenye kujielewa ambazo zina mapungufu madogo madogo yanayohitaji ushauri tu na kuiacha hii blog inayokera nyoyo za watu na kuchafua tasnia ya habari.
ReplyDeleteHuwo uyanga wako peleka kwenye gazeti la bingwa ambalo ulifukuzwa tumecheza mechi zote na tumeshinda wewe na hao kandambili wako mlio pewa goli na huyo refa mechi ya polisi mshukuru mungu kama huna cha kuandika futa hii blog yako
ReplyDeleteYanga wameipiga bao Simba!!!Mechi tatu pointi 4!!Huko ndio kupiga bao??Kweli uzwazwa na ukandambili unaweza kusema chochote .
ReplyDelete