SAMATTA AACHANA RASMI NA UKAPERA
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, amefunga ndoa usiku wa kuamkia (jana) Alhamisi Agosti 10, 2019 huko Mtoni Kijichi jijjni Dar es Salaam na mchumba wake Naima Omary ambaye pia ni mama wa watoto wake wawili.
Harusi hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wacheza soka, wasanii na watu wengi mashuhuri wakiwemo ndugu na marafiki.
Ikumbukwe Samatta aliwahi kusema asingependa kuoa kwa kipindi hiki kwa kuwa angependa kupambana zaidi kisoka.
Hongera sana Kijana. Allah Akufanyie wepesi katika ndoa yako na kwa baraka za ndoa utafanikiwa zaidi katika maisha yako duniani na Akhera In Shaa Allah
ReplyDelete