December 5, 2019


UONGOZI wa KMC umewaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo juu ya afya ya Mohamed Samatta ambaye alipata majeruhi kwenye mchezo wa dhidi ya Yanga.

Samatta aliumia mguu baada ya kuchezwa rafu na nahodha wa Yanga Papy Tshishimbi na kumfanya mwamuzi Elly Sasi kumuonyesha kadi ya njano Tshishimbi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa KMC, Anwari Binde amesema kuwa mashabiki wasiwe na mashaka na Samatta kwani hana maumivu makubwa anaendelea vizuri.

“Samatta alipata majeraha ya kawaida tu kwani licha ya kushindwa kuendelea na mchezo alipewa huduma ya kwanza na sasa anaendelea vizuri, wachezaji wamepewa mapumziko atarejea uwanjani timu ikirudi kambini,” amesema Binde.

KMC imevunja uteja na Yanga ambayo msimu uliopita ilikomba pointi zote sita za ligi kwa kuifunga KMC nje ndani kwenye mechi zilizochezwa uwanja wa taifa baada ya  kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic