March 24, 2020



DEOGRATIUS Munish, 'Dida' mlinda mlango wa Lipuli amesema kuwa bado kikosi chao kina nafasi ya kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu Bara.

Kwa sasa Ligi Kuu Bara imesimamishwa kwa muda ili kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona.

Lipuli ipo nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara imecheza mechi 29 kibindoni imekusanya pointi 33.

Dida amesema:"Wachezaji wanatambua kazi yao ni kutafuta matokeo na ninapokuwa kwenye lango huwa ninapata nafasi ya kuzungumza na mabeki wangu ili kuona namna gani tutapata matokeo chanya,".

Lipuli imeruhusu mabao ya kufungwa 39 na imefunga mabao 35 kinara wa kutupia ni nahodha wao, Paul Nonga mwenye mabao 11 na pasi nne za mabao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic