STAA wa zamani wa Barcelona, Rivaldo
amefunguka kuwa uwepo wa mchezaji Antonie Griezmann ndani ya klabu
hiyo kumemkumbusha uwepo wa Coutinho.
Rivaldo amemfananisha
Griezmann katika msimu wake wa kwanza ndani ya Barca kama ambavyo ilikuwa kwa
Coutinho.
Griezmann amekuwa
akipambana katika msimu wake huu wa kwanza ndani ya Barca lakini bado
inaonekana mambo hayajamnyokea.
Rivaldo alisema: “Unajua
Griezmann ananikumbusha ule msimu wa kwanza wa Coutinho ndani ya Barca, kwa
bingwa wa Kombe la Dunia ambaye tayari anajua soka la Hispania alitakiwa
kuonyesha tofauti hasa baada ya Coutinho kutokuwepo, hakuna Suarez
wala Dembele.
“Nafikiri anatakiwa kuonyesha kitu
cha tofauti kwani Messi hana muda mrefu ndani ya klabu hiyo tunaamini
yeye ndiyo anapaswa kuiga kila kitu kama mbinu na staili za Barca.
“Barcelona ilimsajili kutokana na
ubora wake na yeye anatakiwa kuonyesha utofauti.Hata hivyo Coutinho alitolewa kwa
mkopo kwenda kujiunga na Bayern Munich na msimu ujao anatarajiwa
kurejea.
Griezmann alijiunga Barcelona
akitokea Atletico Madrid kwa kiasi cha euro milioni 120, lakini bado
hajaonyesha cheche zake ndani ya kikosi hicho.
Msimu huu katika michuano
yote Griezmann amefunga jumla ya mabao 13 tu na kati ya hayo nane amefunga
kwenye La Liga.
0 COMMENTS:
Post a Comment