March 25, 2020



DUNIA kwa sasa inasumbuka na janga la kusambaa kwa Virusi vya Corona ambavyo mpaka sasa inaelezwa Italia imechukua vifo vya watu wengi zaidi ya nchi nyingine.

Virusi hivyo ambayo husababisha ugonjwa wa Covid-19, vimefanya shughuli mbalimbali kusimama duniani ikiwemo michezo.

Italia, Ufaransa, Ujerumani, Hispania, Uturuki na nchi zingine barani Ulaya zimesimamisha ligi zao.

Afrika pia mambo yapo hivyohivyo, kuanzia Shirikisho la Soka Afrika (Caf) hadi mashirikisho mengine ya soka kwa nchi mbalimbali yamesimamisha ligi zao.

Afrika Kusini, Morocco, Botswana, Zambia, Kenya, Uganda na hapa nyumbani Tanzania ni baadhi tu ya nchi zilizosimamisha ligi zao lakini kwa jumla ligi za soka zimesimamishwa kwa sasa.

Sababu kubwa ni katika kupambana na janga hili ambalo kwa Tanzania tulitangaziwa lilikuwa limeingia takribani wiki sasa.

Muda mchache baada ya virusi hivyo kuripotiwa kuingia Tanzania, Serikali ikatoa tamko la kuagiza kusitisha mikusanyiko isiyo ya lazima.

Katika hilo, ndipo ikatoka kauli ya kusimamisha michezo kwa siku 30 kuanzia Machi 17, mwaka huu. Miongoni mwa michezo iliyosimamishwa, soka ni mojawapo.

Pia Serikali ikafunga shule na kutoa tahadhari kwa wananchi wake kujikinga na virusi hivyo, pia zikielezwa njia za kukabiliana na kusambaa kwake.

Safari zisizo za lazima za nje ya nchi zimezuiwa. Wananchi wametahadharishwa wasisafiri nje ya nchi kama safari zenyewe hazina ulazima sana, lakini kama utasafiri, fuata maelekezo kutoka kwa wataalamu wa afya ili iwe rahisi kwako kujiepusha kuambukizwa Corona.

 Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) nalo likakazia hapohapo, kusimamishwa kwa ligi zake kukaambatana na kutoa tahadhari kwa wachezaji wa kigeni wasirudi nchini kwao ili tu kuwalinda wao na jamii zao.

Kauli ya Rais wa TFF, Wallace Karia aliyosema itawazuia wachezaji wa kigeni waliokwenda kwao kipindi hiki, inafikirisha sana.

Tangu kauli hiyo itoke, kumekuwa na mvutano, wapo wanaoungana naye, pia wapo wanaompinga.

Yote kwa yote tunapaswa kuelewa kwamba kauli yake ilikuwa ni sehemu ya kutoa tahadhari juu ya janga tulilokuwa nalo.

Hivi itakuwaje ikitokea mchezaji, kiongozi na kocha wa timu fulani hapa Bongo akirudi akiwa na maambukizi hayo halafu akajichanganya na wenzake kabla ya kugundulika. Itakuwa balaa.

Tunaambiwa virusi hivyo vinasambaa kwa njia mbalimbali ikiwemo hewa, sasa huyo mtu akiwa kambini na kujumuika na wenzake kwa muda mrefu, akija kugundulika atakuwa amewaambukiza wenzake wangapi?

Watanzania tuache ushabiki, kwenye mambo siriazi tuwe siriazi kweli, tuache utani.


3 COMMENTS:

  1. Kwanini asiseme kwamba wachezaji wataorudi wapimwe kabla ya kujumiika na wenzao ?Utazuia watu kwenda kwao?Wachezaji wataokwenda Mwanza, Iringa na wengineo wanaotoka timu mbali mbali nani ana uhakika watakuwa salama?Ingekuwa busara TFF iseme timu zipime wachezaji wao wote kabla ya kuanza mazoezi. Wachezaji wengine duniani wamekwenda kwao kwenye kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  2. Baada ya kusimamisha ligi, tamko la wachezaji wasiende makwao halikuwepo bali limetoka baada ya wachezaji wamekwisha enda makwao, mfano tuweke ushabiki pembeni, tangia nianze kuangalia wachezaji na mienendo yao sijawahi kumuona kagere akishtumiwa hivyo najua kama tamko lingetoka mapema sidhani kama kagere angetoka maana ni mtu ambae amekuwa na mienendo ya nidhamu tangia akiwa anacheza ligi nchini kwao mpaka sasa yukko hapa. Hvyo karia atumie busara tamko limetoka tayari wengne wamekwisha ondoka sasa nani alaumiwe?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Chakufanya nikuwataka wachezaji kuchukuliwa vipimo na kusubiri kwa mda wa siku 14 kabla ya kujiunga na wenzao, na huo ndio utaratibu.

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic