MKONGWE ndani ya Liverpool, John Barnes amemshauri staa wa Tottenham Hotspur, Harry Kane kubaki ndani ya timu hiyo.
Kumekuwa na taarifa kwamba nyota huyo anampango wa kuibukia ndani ya Manchester United ili kupata changamoto mpya na kusaka makombe.
"Kane hatakiwi kuondoka Spurs kwa sababu kama anatafuta makombe wachezaji wengi wangehama klabu zao anachotakiwa kwa sasa ni kutulia na kufanya kazi ndani ya klabu yake ya Spurs,".
Spurs kwenye msimamo ipo nafasi ya nane ikiwa imecheza mechi 29 kibindoni ina pointi 41.
0 COMMENTS:
Post a Comment