VIRUSI vya
Corona ambavyo vinasababisha ugonjwa wa COVID-19 kwa sasa vimekuwa janga la
dunia kwa kuibadilisha mambo na kufanya hali ya hofu itawale kila kona.
Kote hofu
imetawala kuanzia kwa wachezaji, mashabiki mpaka makocha pia nao wanahofia
janga hili hapa kuna kitu cha kujifunza kwamba tupo kwenye mapito magumu lazima
tuikubali kwanza hali hii kisha mambo mengine yatafuata.
Serikali kwa
kuligundua hilo ilichukua tahadhari mapema ambapo ilizuia mikusanyiko isiyo ya
lazima na kuwataka watu kwa imani zao wasisahau kufanya ibada ikiwa na maana
kwamba bado kuna nafasi ya kutoka kwenye janga hili iwapo wote tutaungana na
kufanya ibada.
Katika hali
ngumu ambayo wanafamilia wamichezo kwa sasa tunapitia ni lazima tukubali kwamba
kimbilio letu ni Mungu pekee na ibada itatufanya tuwe salama wakati huu na
wakati wote.
Aliyeziumba
mbingu na nchi anajua maumivu ya watu wake ambao amewaumba na anatambua kwamba
wote wanapata maumivu kutokana na janga hili ambalo linaleta hofu na balaa zito
kwa dunia.
Tusisahau
kwamba hata wachezaji nao wamekuwa wakifanya hivi mara kwa mara wanapoingia
uwanjani kwa kufanya sala kwa imani zao na kuendelea na michezo jambo ambalo
linamaanisha kwamba Mungu ni wetu sote.
Nimekuwa
nikizungumza na makocha wengi bila kusahau wachezaji nao pia wamekuwa
wakionyesha jambo la kipekee hasa wakati wa mahojiano wanaanza na Mungu kwanza
kisha mengine yatafuata.
Ipo namna
hii wakati huu tunaopita sio wa kuleta utani ni lazima kila mmoja apambane na
kufuata tahadhari zote za kujikinga na virusi vya Corona.
Kusimama kwa
Ligi Kuu Bara, Ligi Daraja la Kwanza, Ligi ya Wanawake pamoja na masuala yote
yanayohusu michezo inafanya mambo mengi yasimame.
Matokeo yake
yameanza kuonekana kwa wanafamilia za mpira ambapo wafanyabiashara kwa sasa
wamekosa soko la bidhaa zao hasa wale waliokuwa wanamiliki vibanda umiza.
Achana
na wajasiriamali ambao walikuwa
wanategemea kuuza bidhaa zao ili wapate kipato wapo wale wengine ambao furaha
yao kubwa ilikuwa kwenye soka na kuwaona wachezaji wakiwa uwanjani mambo
yamekuwa magumu.
Kikubwa
ambacho wapenda mpira kwa sasa tunatakiwa kukifanya ni kufuata kanuni za afya
na kuendelea kufanya ibada bila kuchoka hili nalo litapita na kila kitu
kitakuwa sawa.
Tukirudi kwa
wachezaji ambao kwa sasa wao watakuwa kwenye mapumziko ambayo yanatarajiwa
kukamilika Aprili 17 kwa sasa wanakuwa wapo huru kufanya mambo yao wanatakiwa
kutobweteka na kuendelea kuishi bila kufanya mazoezi.
Kazi yao
inakuwa ni moja tu kulinda vipaji vyao na kuendelea kuchukua tahadhari wakati
wakifanya mazoezi ya kulinda vipaji vyao ili wabaki kuwa salama wao na familia
zao pia.
Mashabiki
pia wanapaswa kuwa na subira na kuendelea kufuata kanuni za afya huku wakiepuka
mikusanyiko isiyo ya lazima kwa kufuata taratibu ambazo zimewekwa.
Imani yangu
ni kwamba Mungu wetu ataskia maombi yetu na atajibu yale ambayo tunayahitaji
sawasawa na mapenzi yake, Amen .
0 COMMENTS:
Post a Comment