DIEGO Maradona zama zake alitamba na alikuwa ni miongoni mwa wachezaji matata wakiwa ndani ya uwanja.
Ni raia wa Argentina alitamba
miaka ya 80 mpaka 90 akiwa na klabu za Sevilla, Newell’s, Boca
Junior , Barcelona na Napoli, bila kusahau timu yake ya Taifa ya Argentina.
Kwa sasa ni Kocha Mkuu wa Klabu ya Gimnasia de La Plata ya nchini Argentina
Kombe la Dunia alitwaa mwaka 1986 na Kombe la Uefa alitwaa mwaka 1988/89.
Kwenye maisha yake ya soka amecheza jumla ya mechi 491 na ametupia jumla ya mabao 259.
Timu ambazo zilimpa mafanikio makubwa na umaarufu ni Napoli ambapo alicheza mechi 188 alitupia mabao 81 na Barcelona alicheza mechi 36 na kufunga mabao 22








0 COMMENTS:
Post a Comment