April 9, 2020


BADO dunia ipo kwenye giza nene kutokana  na  ugonjwa wa COVID19 wa Virusi vya Corona ambao unaendelea kuitikisa dunia kwa kasi na nchi zikipoteza maelfu ya watu kila kukicha na wengine bado hali mbaya wapo vitandani wakipigania maisha  yao kutokana na janga hili.
 Hakuna asiyejua nini  kinaendelea kwa dunia ya sasa Virusi vya Corona vimekuwa vikimaliza watu bila kuchagua huyu ni nani wala yule ni nani ukipata unakwenda hasa kama utashindwa kujitokeza kwa ajili ya kupewa huduma za afya. 
 Kwenye soka tayari tumeshuhudia viongozi  wa klabu za soka hasa huko Ulaya wamefariki na Virusi vya Corona ambavyo ni tishio kila kona ya dunia  hata  hapa Tanzania.
 Tanzania ni nchi kubwa ambayo ina wakazi wengi waliopo mjini na vijijini lakini licha ya janga hili la Virusi vya Corona baadhi  ya maeneo bado hawajapata elimu kuhusu  janga hili.
 Kama  inavyofahamika soka ni burudani  wakati huu ni muafaka kabisa kwa wachezaji na klabu kwa ujumla kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanakuwa wa kwanza kutoa elimu kwa jamii  zinazowazunguka kuhusiana na virusi vya Corona.
 Tunaamini wao ni watu ambao wanafahamika na kuwa karibu na jamii kupitipia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kipindi kama hiki wanatakiwa kutoa elimu  na wakati mwingine hata kuzunguka kwa tahadhari na kuwaelimisha watu juu janga hili ili kuepusha vifo kama ilivyo Ulaya.
   Kutokana na hali ilivyo kuna ambao watakuwa na uwezo wa kuichangia jamii vifaa kwa ajili ya wagonjwa na wengine watakuwa hawana uwezo huo, lakini elimu ni bure mnaweza kutoa elimu hiyo kwa jamii ambayo imekuwa ikiwazunguka kwa wakati wote.
 Hakika hakuna kinachoshindikana naamini wale mastaa wa Simba, Yanga, Azam, Ndanda, Mtibwa, Mbeya na Namungo  na wengine hasa walioko mjini watatakiwa kupita  hata vijijini kuendelea kuielemisha jamii kuhusu Virusi vya Corona  kwa asilimia 50 elimu mjini imetolewa zaidi.
 Hivyo wachezaji  naomba mjitokeze katika hili kwa kurudisha fadhila kwa jamii ambayo inawazunguka kwa kutoa elimu juu ya Virusi vya Corona kwa manufaa  ya vizazi vyetu pamoja na uchumi wa nchi kwani Virusi hivi vikisambaa kwa kasi vitapoteza nguvu kazi ya watu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic