May 8, 2020



KOCHA Mkuu wa Yanga, Mbelgiji, Luc Eymael, ameweka wazi kufurahishwa na kauli iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli, juu ya kufikiria kuruhusu ligi kuendelea kama kawaida, huku akimtumia ujumbe maalum.

Ligi Kuu Bara na ligi zingine hapa nchini zimesimama tangu Machi 17, mwaka huu kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona.

Eymael ambaye kwa sasa yupo Ublegiji kwa mapumziko, amemuomba Rais Magufuli afungue viwanja vya ndege kwa sababu wachezaji na makocha wa kigeni waliorejea kwao, waweze kurudi Tanzania kuendelea na majukumu yao.

“Nimesikia Rais wa Tanzania akisema anafikiria kuruhusu ligi iendelee, unajua Ujerumani na Italia wanatarajia kuendelea kucheza kuanzia mwezi huu.

“Kwa upande mwingine, naomba rais afungue viwanja vya ndege kwa ajili ya kupokea ndege za kigeni, huku Ubelgiji viwanja vya ndege vinatarajia kufunguliwa wiki ijayo, hata Tanzania inabidi iwe hivyo kwa kuwa baadhi ya wachezaji na makocha wa timu kama Yanga na Azam wanatakiwa warudi kwa ajili ya kumalizia mechi zilizobaki.

“Kikubwa tutakachofanya ni kila timu ihakikishe inawaweka wachezaji hotelini na ikitokea wanasafiri basi wasafiri wakiwa wamejikinga vizuri, uwanjani inabidi uwekwe utaratibu wa kupima wachezaji, makocha, waamuzi na watu wanaotunza viwanja,” alisema Eymael.


SOURCE: SPOTI XTRA

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic