UONGOZI wa
Alliance FC umesema kuwa msimu ujao
watabaki ndani ya Ligi Kuu Bara hawatashuka daraja kushiriki Ligi Daraja la
Kwanza.
Alliance FC
inashikilia rekodi ya kuwa timu pekee iliyompiga chini kocha wao aliyeongoza
ligi ndani ya dakika 90 ambaye alikuwa ni Athuman Bilal, ’Bilo’ kwenye mchezo
wake dhidi ya Mbao FC ambapo iliisha kwa sare ya kufungana bao 1-1.
Akizungumza
na Saleh Jembe,Mwenyekiti wa Bodi mashindano wa Alliance, Yusuph Budodi amesema
kuwa wana imani hawatashuka daraja kutokana na mipango mikali waliyonayo.
“Hatukuwa
kwenye mwendo mzuri hilo lipo wazi lakini kwa hesabu ambazo tunakuja nazo pale
ligi itakaporejea mashabiki wenyewe watatupenda kwani itakuwa ni mwendo wa dozi
tu kwa wapinzani wetu, hatushuki daraja,” amesema Budodi.
Alliance FC
ipo nafasi ya 18 ikiwa imecheza mechi 29 na kujikusanyia pointi 29 imebakiwa na
mechi tisa kukamilisha mzunguko wa pili.
0 COMMENTS:
Post a Comment