May 28, 2020




UONGOZI wa Yanga umesema kuwa hesabu kubwa ni kuona ndoto za safari ya mabadiliko inatimia kwa kuwa ni mpango mkubwa uliopo kwenye majalada ya Yanga.

Yanga imeanza mchakato wa kuelekea kwenye mabadiliko ambapo mchakato huo ulisimama kwa muda kutokana na janga la Virusi vya Corona ambavyo vinaivuruga dunia.

Mshindo Msolla, Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga amesema kuwa ni wakati wa mashabiki na wadau kuunga mkono mpango wa mabadiliko ili kufikia ndoto waliyokuwa wakiiota muda mrefu.

“Imani kubwa ni kuona kile ambacho tunakiota kwa muda mrefu kitatimia kwani tunashirikiana na wadhamini wetu hatua kwa hatua pamoja na wadau mbalimbali, lengo letu ni kuona kwamba tunakuwa kwenye mfumo mpya ambao utakuwa na matokeo chanya kwetu kikubwa ni sapoti,” amesema Msolla.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic