May 10, 2020



GERALD Mdamu, mshambuliaji namba moja ndani ya Mwadui FC  anayeshikilia rekodi ya kuwatungua makipa wote wa Simba, Aishi Manula na Beno Kakolanya amekimbia zake makao makuu ya nchi, Dodoma na kuibukia Songea vijijini kuchukua tahadhari dhidi ya Corona.

Mdamu alianza kumtungua Aishi Manula kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara wakati Simba ikipoteza kwa kufungwa bao 1-0 kisha akamalizana na Beno Kakolanya kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho wakati Mwadui ikifungwa mabao 2-1.

Mdamu amesema kuwa hali haijawa shwari kwa sasa kutokana na hofu iliyotanda dhidi ya kusambaa kwa Corona jambo lililomfanya asepe makao makuu ya nchi.

“Bado mambo hayajawa sawa kwa sasa ni tahadhari na mazoezi, nilikuwa Dodoma ila nimeondoka mpaka huku Songea vijijini ninaendelea kuchukua tahadhari na kufanya mazoezi, nimefurahi kuskia ligi inatarajiwa kurudi hivyo lazima nijiweke sawa,” amesema Mdamu.

Mwadui FC ikiwa nafasi ya 12 na pointi zake 34 kwenye mabao 27 amehusika katika mabao nane ambapo amefunga matano na kutoa pasi tatu za mabao.

 Chanzo ni Championi



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic