May 10, 2020



SVEN Vandenbroeck, Kocha Mkuu wa Simba amechanganywa na dakika 508 za kiungo wa Simba, Miraj Athuman ‘Sheva’ kutokana na data zake kuonyesha kuwa ametumia muda mchache kufanya mambo makubwa uwanjani.

Sheva amefunga mabao sita na kutoa pasi moja ya bao huku akisababisha penalti mbili ndani ya ligi ambapo zote zilifungwa na Meddie Kagere ilikuwa mbele ya Kagera Sugar na Mbeya City.

Sven amesema:”Miongoni mwa wachezaji ambao wanaonekana kuwa bora ni Miraj lakini sijamtumia kutokana na majeraha yake, nina imani akirejea kwenye ubora wake atakuwa na vingi vya kufanya.”

Sheva kwa sasa anatibu jeraha lake la funda la goti ambalo aliumia mwaka jana akiwa na timu ya Taifa ya Tanzania hali yake imeanza kutengamaa. 

Mechi alizocheza ni tisa kati ya 28 ambazo ilikuwa namna hii:-JKT Tanzania (30), Mtibwa Sugar (27) Kagera Sugar, (29), Biashara United (83), Azam FC (33), Singida United, (81), Mwadui (45), Mbeya City (90), Ruvu Shooting (90).

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic