August 29, 2020


ZLATKO Krmpotić kwa sasa ndiye Kocha Mkuu wa Yanga ametua leo mapema akitokea nchini Serbia kuchukua nafasi ya Mbelgiji, Luc Eymael aliyetimuliwa Julai 27.

 

Yanga imemchukua kocha huyo akitokea Polokwane City ya nchini Afrika Kusini huku akiwa amefundisha baadhi ya klabu  kama APR (Rwanda), Zesco United (Zambia) na TP Mazembe (DR Congo).

 

Timu hiyo imemchukua kocha huyo baada ya Mrundi, Cedric Kaze aliyekuwa anafundisha Academy ya Barcelona kupata matatizo ya kifamilia.

 

Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM na Mjumbe wa Kamati ya Mashindano wa Yanga, Injinia Hersi Said amesema :- “Baada ya dili kufeli, haraka tukahamia kwa Zlatko ambaye yeye alikuwa chaguo letu la pili kati ya makocha hao walioleta CV zao Yanga, hivyo kamati ikachukua maamuzi ya kumpitisha Mserbia huyo kuja kuifundisha Yanga,


“Uzoefu wa Zlatko wa kufundisha timu za Afrika ndiyo umetushawishi sisi viongozi kumpa nafasi ya kuja kuifundisha Yanga, kwani aliwahi kuzifundisha klabu za TP Mazembe, Zesco na Polokwane, kocha huyo tumemuachia nafasi mbili za usajili za wachezaji wa kigeni ambazo kama akihitaji mchezaji wake atakayetaka kufanya naye kazi tumsajili,” amesema Hersi.

 

Amewahi kuwa kocha bora kule DR Congo msimu wa 2016-2017, msimu uliofuata pia akawa kocha bora kwenye Ligi ya Zambia akiwa na Klabu ya Zesco pia akawa kocha bora Afrika. Mwaka 2018 baada ya kutua Botswana kuinoa Jwaneng Galaxy aliibuka pia kocha bora wa msimu.

 

"Msaidizi ni Juma Mwambusi ambaye ni mzawa na ni pendekezo la kocha mpya kwamba alitaka kufanya kazi na mzawa.

 

“Pia, kocha wetu mpya wa makipa ni Niyonkuru (Vladimir) ambaye ni raia wa Burundi yupo tayari nchini kwa kufanya kazi yake hiyo, tumeliboresha benchi letu la ufundi kwa ajili ya kufi kia malengo yetu,” alisema Hersi.

17 COMMENTS:

  1. na mwaka 2019-20 kocha wa vibonde wa ligi South Africa

    2017 TP Mazembe Congo
    2018 Zesco Zambia
    2018 Jwaneng Botswana
    2019 APR Rwanda
    2019-20 Polokwane SA

    huyo kocha ni bandika bandua na kwa wale mashabili Eymael aliwaita mbumbumbu na majina mengine.... yetu macho

    ReplyDelete
    Replies
    1. mbona umeanza mbali sana. huyo kocha kuanzia 2013 kila mwaka anakuwa timu nyingine wakati mwingine katika mwaka mmoja timu anakuwa timu mbili.Halafu hao mbumbumbu na gongowazi wamempa miaka miwili ...mwana kulitafuta mwana kulipata

      Delete
  2. Na hiyo Congo kwa TP Mazembe alikuwa assistant ....sasa hiyo honours ya kocha bora aliipataje huku akiwa assistant

    ReplyDelete
  3. 😂😂😂😂 hakuna kocha hapo vichekesho kwa GONGOWAZI aka vyura aka kandambili

    ReplyDelete
  4. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  5. Nyie WE...KUNDU wa Msimbazi mbona mnawashwawashwa sana tuacheni na mambo yetu,hebu wekeni CV ya kwenu hapa tuione inasomekaje halafu tujadili

    ReplyDelete
    Replies
    1. jenga hoja na sio matusi..wengi wanatambua ukivunja neno wekundu sehemu ulipolivunja wewe unapata maneno mawili tofauti na moja wapo ni tusi..au ndiyo wale Eymael alitujulisha kazi yao.
      jenga hoja ingia google tafuta rekodi za Sven weka hapo.Ukweli upo na haufichiki...Sasa huyo kocha mpya tangu 2013 kila mwaka una timu yake..kweli ataweka rekodi endapo atamaliza miwili aliyogawiwa na Yanga

      Delete
  6. Usajili unafungwa tr. 31.8.2020 leo ni 29.8.2020, huu muda utatosha kweli kusajili wachezaji wawili tena wa kigeni?

    ReplyDelete
  7. Ila pimbi wanapenda kuingilia ya watu! Ndo maana mlivyojieungua mkajiita QUEENS! Wanaume mkajiita vile! Ndo maana Mambo yenu ya kiqueen! Mnyama

    ReplyDelete
  8. Mara zote Queens akicheza na gongowazi princess huwa princess anachezea kichapo tu cha wale wanyama aloita Eymael.
    2019 Mechi ya kwanza Simba Queens 5 na Yanga Princess 1 na ya pili Simba Queens 7 Yanga Princess 0
    2020 Simba Queens 3 Yanga Princess 1 na mechi ya pili Simba Queens 5 Yanga princess 1
    Ukweli upo!

    ReplyDelete
  9. Kocha wa Wananchi, Kwann mikia wanateseka?
    Shughuli sio yenu mind your business

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hata mie nawashangaa, badala ya kushughulika na kikosi Chao kilichojaa wastaafu, wanahangaika na jeshi la vijana wa Jangwani

      Delete
  10. Majibu ya CAS bado?Mtandao wa FIFA unaonyesha Morrison mchezaji wa Simba. Kweli hizo milioni 600 tutazipata?Au danganya toto kwa sisi wanachama na mashabiki.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndugu, wewe umeona huo mtandao wa FIFA unaoonesha Morrison mchezaji wa Simba? Usipumbazwe na propaganda za Mikia FC wanaosubiri mchezaji atakiwe na Yanga wao ndo wamwone, kama fisi anayesubiri kubakiziwa

      Delete
  11. Mlisema Morrison ni mchezaji wenu Sasa hizo nafasi mbili zimetoka wapi?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic