August 23, 2020

 

KELVIN Yondani beki mkongwe ndani ya Klabu ya Yanga ambaye aliachwa jumla baada ya mkataba wake kuisha inaeelezwa kuwa yupo kwenye mazungumzo na mabosi wake hao ili arejee kikosini.


Yondani aliachwa pamoja na beki wa kulia Juma Abdul ambao kwa nyakati tofauti ndani ya Yanga waliwahi kuvaa kitambaa cha unahodha.

Sababu ya kuachwa ni kushindwa kuelewana kwenye masuala ya kimkataba jambo lililofanya pande zote mbili kukubaliana kila mmoja aendelee na maisha yake.

Abdul mpaka anaachwa na Yanga baada ya mkataba wake kuisha alikuwa ni nahodha msaidizi.

Habari zinaeleza kuwa kwa sasa mabosi wa Yanga wameanza kufanya mazungumzo na Yondani ili kumrejesha ndani ya kikosi hicho kwa ajili ya kuendelea kupambana kwa msimu wa 2020/21.


Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli hivi karibuni alisema kuwa timu ipo imara kwenye usajili na ikiwa itahitaji saini ya nyota yoyote yule ni rahisi kumpata kwa kuwa wanajiamini.


"Mchezaji ambaye tutakuwa na malengo naye ni rahisi kwetu kumpata kwa kuwa uwezo tunao na tunatambua kwamba malengo yetu yapo kwenye jambo gani, bado tunaendelea na usajili hivyo wachezaji wetu wote tutawatambulisha Agosti 30 Uwanja wa Mkapa,". 


14 COMMENTS:

  1. Wamekosa wachezaji wa nje waliowategemea wamerudi kwa akina yondani. Usitukane mamba ili hali hujavuka mto

    ReplyDelete
  2. Unasemaje uwezo mnao wakati akina yondani walihitaji 30ml tu.

    ReplyDelete
  3. Weye Jana ulicheza na kitimu ambacho kinahistoria kufungwa mechi kibao ukatudanganya eti mechi ya kimataifa��������������

    ReplyDelete
  4. Yondani wa nini tena wakati tuna Mwamnyeto tuliyempa milioni 200 za usajili?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Namshauri Cotton juice atafute changamoto mpya kwenye timu itakaypheshimu kipaji chake. Yanga ilshamwacha asirudi nyuma watamdharau zaidi

      Delete
  5. ukiona hvyo ina mwanyento haminiki hahahahahahha

    ReplyDelete
  6. Dah!utopolo mnaiga wakati hamwezi, ninyi level yenu ni Amina yondani na mkivuka sana zenji na Kenya *utopolo Ni utopolo tu pesa Hamna mjikubali msiige mtaumia.* Wanaume tunacheeeja 😆😆😆

    ReplyDelete
    Replies
    1. Wewe mkiya fc anga zako za mazembe al ahly zamalek lkn usajili wako wote ulofanya wachezaji walomaliza mkataba latika team zao huna uwezo wa kununua wa kuvunja mkataba na hizo team

      Delete
  7. Hao wachezaji wasio na uchungu na timu wanarudishwa kwa nini?!!

    ReplyDelete
  8. Yondani; Juma Abdul na Ngasa walipaswa kuachwa kwa heshima siyo hivyo walivyofanyiwa.

    ReplyDelete
  9. Wanakula matapishi yao tena hawana lolote hao kandambili aka vyura aka GONGOWAZI

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic