September 5, 2020



KESHO Jumapili, Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21 unatarajiwa kuanza ambapo zitachezwa mechi saba, kisha Jumatatu zitamalizia tatu kukamilisha raundi ya kwanza.

 

Jumla ya timu 18 zitashiriki ligi hiyo kwa msimu huu ambapo zimepunguzwa kutoka 20 zilizokuwa kwa misimu miwili iliyopita.

 

Punguzo la timu limekuja likiwa na lengo la kuona ushindani unakuwa mkubwa zaidi, hii ni baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuona kuwa na lundo la timu halafu zingine zinalia njaa, si sawa.

 

Kikubwa kila mmoja wetu anahitaji kuona ushindani kuanzia ndani hadi nje ya uwanja. Hayo yote yanawezekana kama timu zote zitajimudu.

 

Kuwa na lundo la timu kwenye ligi kisha mambo yakaenda ndivyo sivyo, ndiyo mwisho wa siku tunakuja kushuhudia timu zingine zikiwa hatarini kumaliza ligi kwa sababu ya ukata.

 

Mifano ipo mingi, hii ishu ya timu kushindwa kujimudu katika ligi na kuanza kulialia njaa lipo kwa misimu mingi. Lakini kwa misimu miwili iliyopita lilikithiri sana, hivyo basi imani yangu ni kwamba msimu huu hatutakuwa na vilio vingi.

 

Wadhamini wakuu wa ligi hiyo, Kampuni ya Vodacom, kwa miaka mingi wamekuwa wakiidhamini ligi hiyo kiasi cha kuondoa yale makali ya klabu kujiendesha, lakini ilipojiweka kando, hali ilikuwa mbaya sana.

 

Kuanza kwa ligi hapo kesho, kuwe na mambo mengi mapya, wadau wa soka tunahitaji kuona mabadiliko makubwa sana kuanzia kwa wachezaji, mabenchi ya ufundi hadi mashabiki.

 

Kwa wachezaji, mnapaswa kucheza kwa viwango vya juu, kuwa kwenye kikosi cha timu uliopo kwa sasa si kwa bahati mbaya, makocha wameona uwezo kwamba unaweza kuisaidia timu, hivyo lipa imani hiyo kutoka kwa makocha wako.

 

Itakuwa ni aibu kwako kucheza kama umelazimishwa wakati hiyo ni kazi yako. Kila mmoja aifanye kazi yake ipasavyo, hapo mtaona matunda mazuri ndani ya timu yenu.

 

Kwa benchi la ufundi, suala la kupanga kikosi liwe la kufuata weledi, kusiwe na vinyongo kwa sababu tumekuwa tukisikia sana kwamba wachezaji wakiwa na sintofahamu na makocha wao, basi benchi linakuwa makazi yao.

 

Kikubwa suala la ugomvi wenu wa nje ya uwanja msiulete kwenye timu, itawagharimu sana tu, linapofika suala la kazi, wekeni tofauti zenu pembeni, mtafanikiwa.

 

Mashabiki na nyinyi muwe na umoja na mshikamano katika kuzisapoti timu zenu. Hakikisheni mnakuwa kwa wingi viwanjani kuwapa sapoti wachezaji wenu wawape matokeo mazuri.

 

Wachezaji wanapenda kuona mashabiki wao wanavyowasapoti, hapo huwa na nguvu zaidi ya kupambana kuwapa matokeo mazuri ili mfurahi.

 

Kuna kauli ya kwamba shabiki ni mchezaji wa 12, hivyo ikitokea mechi inachezwa halafu mashabiki hawatoi sapoti, wachezaji wanashuka morali, mwisho wa siku wanapoteza mechi.

 

Lakini ikitokea siku timu imepoteza mechi, msianze kunyoosheana vidole, kaeni chini na muangalie wapinzani wenu wapi waliwazidi nguvu, kisha jipangeni kwa wakati ujao.

 

Kupoteza mechi moja si mwisho wa safari, mnaweza kujipanga na kufanya vizuri mechi zinazofuata, mwisho wa siku mnafikia malengo.

 

Yote kwa yote niwatakie kila la heri katika mechi zenu na msimu kwa jumla. Tunataka kuona mabadiliko ili soka letu likue zaidi.

5 COMMENTS:

  1. Timu ziache visingizio. Ukifungwa kubsli matokeo. Baadhi ya timu ziache kudanganya wapenzi na wanachama wao.Tuanze utamaduni wa kusema ukweli.Tambo za magazetini hazileti ushindi.

    ReplyDelete
  2. Kwa mawazo yangu; hiyo ligi bora ingechezwa Leo na kesho kuliko jumatatu.
    Jumatatu ni siku ya kazi tena ya mwanzo wa wiki, bodi ya ligi huwa siwaelewi kabisa

    ReplyDelete
    Replies
    1. Bodi ya ligi sijui ilikuwa inafikiria nini

      Delete
    2. Na Kuna Jambo kingine la Venue ya fainali ya kombe la TFF. Unapopanga uwanja wa mikoa ya Katavi au Njombe,au Mara na mashindano yanahusisha timu za madaraja ya chini, what if zikaja kuingia fainali Kati ya timu hizo na mchezo ulishapanga kufanyika labda Kigoma?
      Kwa mtazamo wangu Venue yafya ingekua uwanja wa Mkapa then hizi timu ndogo zinakua zinapambana kucheza hapo Kama kivutio na motivation kwao.

      Delete
    3. Vilabu vyote ni sehemu ya bodi ya ligi hivyo vilishirikishwa kwa namna moja au nyingine kwenye maamuzi ya ratiba

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic