October 19, 2020


 

KOCHA Mkuu wa Biashara United ya Mara, Francis Baraza amesema timu yake imejipanga kuhakikisha inapata matokeo katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union utakaochezwa leo Jumatatu mkoani Tanga.

 

Baraza amesema: “Kwa sasa naweza kusema najenga nyumba mpya baada kupata matokeo nyumbani. 


"Tumejipanga kushinda dhidi ya Coastal, tunaamini utakuwa mchezo mgumu kwani timu hiyo haijafanya vizuri tangu kuanza kwa ligi ya msimu huu, tutajipanga kupata matokeo mazuri ambayo yataiweka timu yetu kwenye nafasi za juu zaidi.

 

“Tutachukua tahadhari zote za kucheza ugenini lakini shabaha kubwa ni kupata mabao mengi katika mchezo huo.Kwa sasa kama timu tumeamua kila mchezo uwe fainali kwa kuhakikisha tunapata matokeo kwenye kila mchezo." 


Juma Mgunda, Kocha Mkuu wa Coastal Union amesema kuwa wana kazi kubwa ya kufanya ili kurejea kwenye ubora kwa kuwa mwendo wao umekuwa ni wakusuasua.

 

 Biashara United ipo nafasi ya nne kwenye msimamo baada ya kucheza mechi sita na kujikusanyia pointi 13 inakaribishwa na Coastal Union iliyo nafasi ya 14 na pointi zake tano baada ya kucheza mechi sita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic