November 5, 2020




 IMEBAKI
 siku moja kuanzia sasa kabla ya kuchezwa ile mechi ya watani wa jadi ambayo inasubiriwa kwa shauku na wadau ndani ya Bongo ile ya Yanga na Simba.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Novemba 7 Uwanja wa Mkapa na tayari kwa sasa viingilio vimewekwa wazi hivyo kila mmoja yupo na chaguo lake akijua kwamba wapi atakwenda kukaa.


Mbali na kutambua viingilio pia maandalizi kwa timu zote naona yanaendelea kwa kuwa ili timu iingie uwanjani ni lazima ijipange kufanya kweli kabla ya mechi.


Kikubwa ambacho kinatakiwa ni mashabiki, wachezaji kuamini kwamba hakuna timu yenye uhakika wa kushinda kila timu ina nafasi ya kushinda ikiwa itafanya maandalizi mazuri.


Masuala ya kuingia na matokeo uwanjani muda wake umekwisha dakika 90 zitaamua nani ni nani na kwa nini apate matokeo hayo.


Atakayeshinda atajulikana baada ya dakika 90 ikiwa ni mwenyeji Yanga sawa ama Simba mgeni sawa hata sare pia inawezekana kikubwa ni kwa timu zote kufanya maandalizi mazuri.

Waamuzi ambao watapewa kazi ya kuchezesha mchezo huu wana jukumu la kuwa makini katika kutimiza sheria 17 kwa kuwa kwa mechi za hivi karibuni wengi wamekuwa wakivurunda.


Sehemu ya kona iwe kona, sehemu ya faulo ipigwe tu hakuna tatizo na penalti pia zitolewe zile halali na sio ilimradi penalti, kikubwa ni umakini ili kuepuka lawama.


Nina uhakika Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) litakuwa na umakini katika hili kwa kusimamia kila kitu kiende sawa na isiishie kwenye mechi za Yanga na Simba pekee hapana lazima iwe kwenye mechi zote za ligi.


Kila mchezo ambao unachezwa uwanjani unahitaji kutazamwa kwa umakini na waamuzi nao wana jukumu la kufuata sheria 17 za mpira ndani ya uwanja.

Kuna kasumba yakuzitazama kwa ukaribu hizi mechi za dabi jambo ambalo linadumaza soka letu. Muhimu kwa kila timu kupewa kipaumbele na kuona kwamba kila timu ni sawa ndani ya uwanja.


Kwa upande mwingine sasa tayari ligi kuu imezidi kushika kasi kwa kuonyesha ushindani mkubwa.Rai yangu kwa timu zote kuhakikisha kwamba zinapambana na kufanya maandalizi mapema.


Tumeona kwenye upande wa usajili wapo ambao wamefanya vizuri na wengine wamebuma kikubwa ni timu katika hili ni kuwaandaa pia watu wa scauti iliwaweze kuwatambua wachezaji ambao watawasaidia wakati wa dirisha la usjili wasipate tabu kama wakati mwingine.


Maandalizi kwa kila timu yanapaswa kuwa mapema na sio ya kukurupuka kwa kuwa matokeo yake huwa hayawi mazuri hata mara moja hivyo muda ni sasa kwa kila timu kulitambua hilo.


Ushindani unaleta raha hasa kwa matokeo ambayo yanapatikana inaonesha kabisa kwamba timu zote zimejipanga kiasi cha kutosha hakuna mnyonge licha ya changamoto ambazo haziwezi kuzuilika.


Waamuzi yawapasa kuongeza umakini ndani ya uwanja kwa kuwa tayari tumeanza kuona lawama ambazo znatokea mara kwa mara kwa ajili yao hivyo ili kuzidisha utamu wa ligi yawapasa wawe nao makini pia.


Jambo lingine ni kuhusu Ligi Daraja la Kwanza ambayo imekuwa ikiwekwa nyumanyuma kama mfuko wa koti hasa katika uangalizi wake na usimamizi wake.


Kwa kweli mazingira ambayo wanayapitia sio rafiki kwa kuwa kuanzia miundombinu mpaka vifaa vyote ni vya chini zaidi hivyo kuwafanya wengi kuandelea kushiriki mashindano haya kwa kuungaunga jambo ambalo linaua uwezo wa timu zetu.


Timu ili iwe bora ni lazima ipate maandalizi mazuri hata ligi ambayo inashiriki pia yapaswa kuwa na ushindani hali ambayo itasaidia kuweza kupata mshindi wa kweli hapo baadaye mara baada ya kupanda daraja.


Timu ambazo zinashiriki Ligi Daraja la Kwanza ndizo ambazo zikipata nafasi zinashiriki ligi kuu hivyo zinapaswa nazo pia ziwe na waangalizi ambao watazisaidia katika kupambana ili zikipanda daraja ziweze kuwa na ushindani ule ule na sio kuanza kuyumba.


Katika kufanikisha hilo ni wajibu wa bodi ya ligi kuandaa mazingira kwa ajili ya timu ambazo zinashiriki Ligi Daraja la Kwanza kuweza kuwa na mdhamini ambaye atasaidia kuongeza ushindani.


Kwa kufanya hivyo kutaongeza hamasa za timu shiriki kuweza kujiandaa mapema hata kabla hazijapanda kwa kuwa kutakuwa na ushindani wa kweli katika kila hatua ambayo wanapitia na kuweza kufanya kusiwe na tofauti kubwa muda watakaopanda daraja.


Pia itarahisisha kwa timu kuweza kuwa na mahusiano mazuri na kampuni mbalimbali hali itakayosaidia kuweza kupata wadhamini kutoka sehemu tofautitofauti hata pale ambapo watapanda daraja kutoka pale ambapo walikuwa awali kiushindani.


Kila kitu kikiwa kwenye mpangilio imani yangu ni kwamba ule muda wa kuwa wasindikizaji utakuwa umekwisha na badala yake tutakuwa na vipaji ambavyo vitasaidia kukuza vipaji wa timu zetu pamoja na ushindani.


Kitu cha kuzingatia ni kuhakikisha kwamba kila mmoja anatimiza jukumu lake kwa wakati bila kutegeana na kukumbushana kwamba maendeleo ya mpira hayaji ghafla bila kutarajiwa ni lazima kuwe na mikakati imara ambayo itasaidia kuwa na sera ambazo zitazaa matunda.


Hakuna mafanikio ambayo hutokea kwa bahati mbaya bali ni kupitia kujituma na kuhakikisha kwamba vile vipaji ambavyo vinakuzwa na kulindwa na sio kupotea bila kuwa na malengo yoyote itatufanya tuzidi kuwa wasindikizaji kila siku.

 

Dabi iwe ya haki na mshindi ambaye atapatikana ni yule ambaye amejipanga vizuri kila timu ina nafasi ya kushinda, kufungwa hata kupata sare kikubwa ni maandalizi mazuri na kuacha suala la kubeba matokeo mfukoni.

7 COMMENTS:

  1. Apigwe 5 kandambili aka vyura aka GONGOWAZI tuufunge mwaka inshaallah

    ReplyDelete
  2. Kuma we , 5 atapigwa mama yako, nguruwe fc wewe

    ReplyDelete
    Replies
    1. Acha matusi wewe tushakupiga tano Mara ngapi mpaka sasa. Tunakupiga tena Kama Kama kawaida yetu kuwachapa tano.

      Delete
  3. Achen matusi toeni hisia zenu sio matusi bado mwamuzi atakuwa dk 90

    ReplyDelete
  4. Yanga wamekuja wakati mbaya sana, yaani watapigwa manyani hawa hadi watamkumbuka Luc Eymael, maana walau alishaanza kuwajengea wachezaji uelewano. Huyu Mrundi amekuja ni kama anaheshimiwa tu, ila bado timu haieleweki vile, kichaka kilichopo ni kauli kwamba 'kocha apewe muda'

    ReplyDelete
  5. Sasa matusi ya nini nyie wadau, badilikeni acheni ushabiki wa kishamba huo. Matusi hayana nafasi ktk mpira, cc ni watani Wa jadi na si mahasimu, naomba tuelewane.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic