BADO fungiafungia ya viwanja kwenye ardhi ya Bongo inaendelea jambo ambalo linazidi kuleta hisia mpya kila iitwapo leo kwamba awali wakati vinaanza kutumia nani aliruhusu viweze kutumika?
Kwa kinachofanywa na Bodi ya Ligi Tanzania,(TPLB)
kufungia vile viwanja ambavyo havina ubora ninawapa pongezi kwa kuwa ili
wachezaji wafanye kweli ni lazima pia hata sehemu wanayochezea nayo iwe rafiki.
Wengi walikuwa wanafuatilia sehemu za kukaa
wachezaji wa akiba pamoja na mashabiki huku sehemu ya kuchezea ambayo ndiyo
inaleta matokeo chanya ilikuwa ikipewa kisogo
Tumeshuhudia kwamba baadhi ya viwanja ambavyo
awali vilifungiwa na TPLB kuweza kutumika vimefanyiwa maboresho na kwa sasa
angalau vinaleta picha nzuri kwa kuwa muonekano wake umekuwa bora.
Karume wa Mara ambao unatumiwa na Klabu ya
Biashara United, Gwambina Complex wa Mwanza ambao unatumiwa na Gwambina wenyewe
ni miongoni mwa viwanja ambavyo vimefanyiwa maboresho.
Kikubwa ambacho kinatakiwa kwenye viwanja ambavyo
vimeboresha ni kuendelea kuongeza juhudi na kuvifanya viwanja hivyo vizidi kuwa
bora muda wote ili viendelee kutumika kwenye matumizi mengine.
Tunaona kwamba taratibu kuna mabaoresho ambayo
yameanza kuonekana na wachezaji nao wameanza kuonyesha kwamba mabadiliko hayo
yana faida kwao hasa katika suala la kupambana ndani ya uwanja.
Ile fungiafungia iwe somo kwa timu nyingine
ambazo zinamiliki viwanja kwa kufanya maboresho kwenye sehemu ambazo hazipo
sawa ili kuepuka adhabu.
Niliweka wazi siku moja hapa juu ya ugumu wa
Uwanja wa Mkwakani katika kusaka matokeo pamoja na Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
mambo yalikuwa ni magumu kwa wakati wake.
Kwa kuwa wakati huu vimefungiwa ni fursa kwa
wamiliki kuweza kuuboresha ili uweze kutumika kwa wakati ujao pindi utakapokuwa
umekamilika.
Itakuwa ngumu ikiwa hakutakuwa na maboresho
kuweza kuruhusiwa kutumika tena kwa kuwa mamlaka imeeleza kuwa itafanyia
ukaguzi kabla ya kuruhusu uwanja kutumika.
Gharama za uendeshaji kwa timu ambazo zimeshazoea
kutumia viwanja vyao ambavyo vimefungiwa hapo lazima itaongezeka hivyo ili
kupunguza gharama ni lazima kwa timu husika kufanya ukarabati kwa upesi.
Msimu huu wa 2020/21 tunaona kwamba viwanja vingi
vinakutana na adhabu kwa kufungiwa ili kufanyiwa maboresho ni muhimu kufuatilia
pia namna ya kuboresha viwanja na sehemu za kukaa watazamaji kwa ajili ya kuona
kwamba msimu unamalizka kwa aina ya kipekee.
Ndani ya uwanja ushindani umekuwa mkubwa na kila
timu inapambana kupata matokeo hilo ni jambo la msingi kwa kila mmoja.
Pongezi kubwa kwa wachezaji wa timu zote ambao
wanapambana kwa wakati huu ni kuona kwamba wanaweza kufikia malengo ambayo
wamejwekeea.
Mashabiki wengi wanazidi kujitokeza uwanjani na
wameona ushindani na soka tamu ambalo wengi wanapenda kuliona siku zote hicho
ndicho kikubwa tunachohitaji kwenye soka.
Kikubwa ambacho kinahitajika ndani ya uwanja ni
kuweza kutafuta ushindi kwa juhudi zote ili kuweza kufikia malengo ya timu
ambayo imejiwekea.
Ikitokea tofauti na hapo na kuanza kuleta porojo
na maneno kushindwa ni karibu kwa timu ambayo itashindwa kujiandaa vizuri na
kuleta maneno mengi.
Sasa hapo ndipo utagundua kwamba mpira ni
uwanjani maneno maneno hayasaidii kukuza soka letu, kila mmoja kwa wakati wake
anapaswa kutimiza majukumu yake.
Kosa moja likalofanywa na timu litawagharimu na
kuacha pointi tatu ziende kwa wapinzani. Haya ndiyo maisha ya mpira kila mmoja
anapambana kutumia makosa ya mpinzani wake.
Muda wote wachezaji mnapaswa kuwa makini na
wapinzani wenu ili kulinda matokeo na pia katika kupata matokeo ni lazima kila
mmoja atumie kosa la mpinzani kupata ushindi.
Benchi la ufundi lina kazi la kutengeneza timu
imara na yenye ushirikiano ambayo inaweza kutoa matokeo kwenye mechi zote ndani
ya ligi.
Ule uzembe wa wachezaji pamoja na kushindwa
kuheshimu mechi zilizo mbele ni chanzo cha kushindwa kupata matokeo mazuri.
Kila kipindi kina mbinu zake, wapo ambao wamekuwa
wakifanikiwa kipindi cha kwanza na kufeli kipindi cha pili na wapo ambao
wanafeli vipindi vyote viwili kikubwa ni maandalizi.
Ukitazama kuna timu ambazo kipindi cha kwanza huboronga na kuna timu ambazo huweza kufanya vizuri. Zipo ambazo zinafanya vizuri mwanzo kisha zinapotea jumla.
Kuna ushindani mkubwa kwa sasa kwenye ligi na
wachezaji wanapaswa wajitambue wasibweteke na mafanikio ya muda wanayopata ama
kuvunjika moyo kwa matokeo mabaya.
Mpira hautabiriki kila mmoja ana nafasi ya kupata
matokeo bila kujali yupo vipi jambo la msingi tu awe amejiandaa sawasawa.
Kwa timu ambazo zimekuwa na mwenendo mbovu benchi
la ufundi lifanye kazi ya kurekebisha makosa na kutumia mbinu mpya kupata
matokeo.
0 COMMENTS:
Post a Comment