VIUNGO
wawili wa kikosi cha Yanga, Saido Ntibanzokiza na Tuisila Kisinda chini ya
Kaimu Kocha Mkuu, Juma Mwambusi wamepewa mikoba ya kiungo Muangola Carlos
Carlinhos.
Ndani ya
kikosi cha Yanga, Carlinhos alikuwa anaaminika kwa kupiga mipira iliyokufa ikiwa
ni kona pamoja na faulo na ana pasi mbili za mabao ambazo zilitokana na mipira
hiyo ila juzi alikosekana kwenye mchezo wa ligi dhidi ya KMC jambo lililofanya
mikoba yake kuwa mikononi mwa Kisinda na Saido.
Wakati ubao
wa Uwanja wa Mkapa, ukisoma Yanga 1-1 KMC, Saido alipiga jumla ya faulo 10 na
moja kati ya hiyo ilileta bao lilifungwa na Yacouba Songne dakika ya 46.
Kwa upande
wa Kisinda yeye alipiga jumla ya kona 4 ambazo zote zilikuwa zinaanuliwa
jumlajumla anga za KMC na Andrew Vincent, ‘Dante’ ambaye alikuwa kwenye ubora
wake.
Mwambusi
amesema kuwa aliamua kuwabadilishia majukumu wachezaji
wake kwa sababu anahitaji kutengeneza muunganiko mzuri katika kikosi hicho.
0 COMMENTS:
Post a Comment