NGOMA inapigwa kwa kasi kwenye ligi kwa sasa ikiwa ni mzunguko wa pili na kila mmoja anapigania malengo yake ili kupata kile anachostahili.
Bado
vita ya ubingwa ni mbichi kwa sasa ambapo zile zilizo tatu bora zinapewa nafasi
ya kumtoa mbabe ambaye atasepa na taji hilo lenye thamani kubwa kwa timu.
Kuna Simba ambao ni vinara, wapo Yanga nafasi ya pili na Azam FC hapo wamejikita
nafasi ya tatu bado wanazidi kutuniashana misuli kuona kwamba nani anasepa na
ubingwa.
Ipo
wazi kwamba bingwa mtetezi ambaye ni Simba naye malengo yake ni kuona anaweza
kutetea taji hilo huku Yanga nao wakiweka wazi kwamba wanahitaji kulitwaa taji
hilo baada ya kulikosa kwa muda mrefu.
Azam
FC pia wao mdogomdogo wanasema kwamba wana jambo lao ambalo wanahitaji kutimiza
hivyo kwa kuwa kila mmoja ana mechi mkononi ni suala la kusubiri na kuona.
Kama
ilivyo ngumu kwenye ubingwa pia ni ngumu kwenye kushuka daraja pamoja na zile
ambazo zitamaliza ndani ya 10 bora mchakato ni mkubwa na kila timu inahitaji
ushindi.
Naona
kwamba wengi wanashangaa imekuajekuaje Simba ikashinda bao 1-0 mbele ya Mwadui
FC tena kwa mbinde ilihali timu hiyo ipo nafasi ya 18 ikiwa inapambana kubaki
kwenye ligi msimu ujao?
Huu
ni mpira na kila timu inastahili kushinda hivyo hakuna timu ambayo inapaswa
kufungwa wala ambayo inapaswa kushinda muda wote.
Ikiwa
hivyo basi isingekuwa na umuhimu wa kuwepo kwa mechi basi zile timu ambazo
unadhani zinastahili kushinda zingekuwa zinakaa pembeni na kuziacha timu
nyingine kushiriki. Kwa kuwa ni mpira basi ni lazima mchezo uchezwe.
Pongezi
kwa Mwadui ila ninawapa neno kwamba walikuwa na kazi ya kuanza kwa gia hiyo
tangu awali. Tunajua kwamba uchumi ni tatizo kubwa linalosumbua timu zetu ila
kwani waliwezaje kucheza mbele ya Simba kwa kasi ile?
Kumbuka
pia waliweza kucheza vizuri pia mbele ya Azam ambayo nayo ipo ndani ya tatu
bora maana yake ni kwamba kila kitu kwenye soka kinawezekana.
Jambo
kubwa ambalo ningependa lifanyike katika mechi hizi za mwisho ni lazima kuwe na
usawa na mechi zichezwe kwa kufuata sheria 17 za mpira.
Mtu
ashinde kwa kutumia nguvu zake mwenyewe na hakuna ujanjanja ambao utafanyika
kwani tunahitaji kuona kwamba kila kitu kinakwenda sawa.
Lala
salama kwa timu zote iwe ni ndani ya Ligi Kuu Bara pamoja na Ligi Daraja la
Kwanza ni muhimu kuweza kuona kwamba kila timu inashinda kwa haki.
Katika
hili ipo wazi kwamba ni jambo la msingi kupata mshindi ambaye hatapata tabu akipanda
ligi msimu ujao wa 2021/22 itasaidia kueleta ushindani mkubwa .
Kwa
kuwa hizi ni mechi za mwisho na zina umuhimu mkubwa kwa kila timu kupata
matokeo mazuri ambayo yatawafanya wafikie malengo waliyojiwekea.
Kikubwa
kinachotakiwa kwa sasa ni kuona kwamba kila timu inafanya maandalizi mazuri ili
kupata matokeo mazuri ndani ya uwanja ambayo yatawapa kile ambacho
wanakihitaji.
Wapo
ambao wamekuwa wanapenda kuleta ugomvi ndani ya uwanja hayo yamepitwa na wakati
ni muhimu kutulia na kufanya maamuzi kwa akili zaidi.
Hivyo
wale wote ambao watakuwa uwanjani wapambane kutafuta matokeo ndani ya uwanja
kupata matokeo chanya.
Kwenye
Ligi Daraja la Kwanza tunataka kuona kwamba kila mechi inakuwa na mvuto pamoja
na ushindani ule ambao unaonekana kwa kila mmoja kucheza na kupata ushindi.
Tunataka
kuona kila timu inapata matokeo ambayo yanastahili kwao na wakimaliza kucheza
wafurahi kile wanachokivuna na baada ya kushuka ama kupanda wasiwe na
malalamiko.
Mechi
za lala salama ni muhimu maandalizi yakawa mazuri katika kumalizia mechi hizi
ambazo zimeshikilia maamuzi ya mechi za mwisho.
Tukija
Ligi Kuu Bara ni muhimu kwa kila timu ikawa na uhakika wa kushinda mechi zote
za nyumbani na ugenini bila mashaka yoyote.
Ipo
nafasi ya kupata matokeo na kujinusuru kwa timu ambazo zina mechi mkononi ikiwa
zitachanga vema karata zao kwa mechi ambazo zimebaki.
Ikiwa
kila mmoja ataamua kufanya vizuri na akapata matokeo mazuri basi zitatimiza
ndoto za kubaki kwenye ligi kwa ajili ya msimu ujao na ikishindikana basi
zijipange kwa ajili ya maisha ya Ligi Daraja Ligi Daraja la Kwanza.
Kwa
zile ambazo zitapanda mpaka kufika ndani ya Ligi Kuu Bara ni lazima zijipange
vizuri katika mechi zote ambazo watakutana nazo kwenye maisha mapya wakati
ujao.
Tunataka
kuona timu zenye ushindani ndani ya Ligi Kuu Bara na zile ambazo zitashuka
daraja zikapambane pia ili kurudi huku ndani ya ligi.
Wasijisahau
kwamba wanakwenda kwenye makazi mapya na wengine wanapanda kwenye makazi mapya
ni lazima kujipanga vizuri hakuna namna.
Wachezaji
wapambane ndani ya uwanja kwa hali na mali kwa ajili ya timu zao ambazo
zinahitaji matokeo mazuri muda wote.
Itakuwa
vizuri ikiwa kila mmoja atakuwa kwenye kutimiza majukumu yake na apambane
kwelikweli kwani ndio kazi yake aifanye kwa ukamilifu bila ulegevu.
Imani
yangu ni kwamba zile ambazo zitashuka zitakuwa zimejifunza na zitakuwa
zimeshuka kwa haki huku zile ambazo zitapanda nazo zinapaswa kupanda kwa haki
bila dhuluma.







0 COMMENTS:
Post a Comment