July 2, 2021

MICHUANO ya Euro 2020 inazidi kupamba moto barani ulaya ambapo sasa ipo katika hatua ya robo fainali, tayari wachezaji mbalimbali wamefanikiwa kuandika rekodi zao katika michuano hiyo, lakini hii hapa ni orodha ya mastaa waliokimbiza zaidi kwa timu nane zilizoingia robo fainali;

Ubelgiji

Romelu Lukaku. Straika wa klabu ya Inter Milan amekuwa katika kiweango bora ndani ya michuano hii. Ameonyesha wastani mzuri wa matumizi ya nguvu na utulivu wake mbele ya lango umekuwa ukiwapa wakati mgumu walinzi wanaopambana naye. Mpaka sasa amefunga mabao matatu hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya kuibuka na kiatu cha ufungaji bora.

Italy

Jorginho. Huyu ni kiiungo wa klabu ya Chelsea ambaye mara kadhaa amejikuta akikosolewa sana uchezaji wake, ameisaidia sana Italy kupata uwiano mzuri katika eneo la kiungo.

Jamhuri ya Czech

Schick. Nyota wa kikosi cha Bayer Leverkusen mwenye miaka 25 ambaye amefanikiwa kuonyesha uwezo mkubwa wa kufunga kwenye michuano hii, Schick pia amekuwa kiunganishi kizuri katika mfumo wa uchezaji wa timu ya Taifa ya Czech.

Denmark

Kinda Mikkel Damsgaard mwenye umri wa miaka 20 anayekipiga kama kiungo ndani ya kikosi cha Sampdoria. Bila shaka watu wengi walikuwa hawamfahamu kabla ya michuano hii ya Euro.

Lakini amekuwa nyota aliyewaka kiasi cha kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuziba pengo la kiungo, Christian Eriksen. Mpaka sasa Damsgaard pia amefanikiwa kufunga miongoni mwa mabao bora kwenye michuano hii, katyika mchezo wao dhidi ya Russia.

Ukraine

Andriy Yarmolenko. Huyu ni winga wa kikosi cha West Ham ambaye amekuwa mara kwa mara akisumbuliwa na majeraha. Ndani ya kikosi cha Ukraine huyu ndiye amekuwa mchezaji muhimu zaidi hasa anapokuwa kwenye robo ya mwisho ya uwanja.

Kwa sasa anakamatia nafasi ya pili kwenye msimamo wa wafungaji bora wa muda wote kwenye kikosi cha Ukraine akiwa ameweka kambani mabao 42.

England

Sterling ni kama vile amelipa heshima aliyopewa na kocha wa England Southgate, hii ni baada ya kufanikiwa kuiongoza vyema England akifunga mabao matatu mpaka sasa, Kwa sasa ni miongoni mwa wachezaji hatari zaidi wa England.

Hispania

Pedri, Kwa sasa ana miaka 18 tu, hiki ni miongoni mwa vipaji bora zaidi kwa klabu ya Barcelona na timu ya Taifa ya Hispania katia siku za usoni.

Amefanikiwa kucheza dakika zote katika michezo minne ambayo Hispania wamecheza mpaka sasa.

Switzealand

Breel Embolo. Huyu ni mwanamichezo wa kweli, akiwa na miaka 24 tayari nyota huyu amekuwa akizivutia klabu mbalimbali ambazo zinatarajiwa kutuma ofa zao kwa klabu ya Borussia Monchengladbach inayommiliki. Amefunga bao moja kwenye mchezo dhidi ya Wales.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic