October 10, 2021


 YANGA watabaki kwenye kambi yao iliyopo Avic 
Town Dar baada ya uongozi kuamua kufuta ratiba ya kwenda kuweka kambi Arusha kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya Ligi Kuu Bara.

Uongozi wa Yanga umeshtukia ratiba yao ya kuweka kambi Karatu wakiona ni kama watapoteza muda kwa kuwa muda uliobaki ni mchache na itakuwa vizuri kama wakibaki Dar na kuepusha gharama zisizo na msingi.


Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga, Thabity

Kandoro, ameliambia Championi Ijumaa: “Timu

itabaki Dar es salaam ikiwa kwenye kambi yetu

ya Avic Town, baada ya kufikia uamuzi wa

kusitisha safari ya kwenda Arusha kuweka

kambi.


“Kubaki hapa kutaipa timu nafasi ya kupumzika

na kuwapunguzia uchovu wa safari za hapa na

pale, lakini pia hapo kuna ishu ya gharama.”


Yanga inajiandaa na mechi ya tatu ya Ligi Kuu

Bara dhidi ya KMC itakayopigwa Uwanja wa

Majimaji, Songea mkoani Ruvuma Oktoba 19 na

sasa wamekuwa wakitenga muda wa kuingia

Gym.

Leo Oktoba 10 inatarajiwa kuwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya JKU SC unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, saa 1:00 usiku.

4 COMMENTS:

  1. Viongozi wetu wanakurupuka sana katika kutoa maamuzi. Walikuwa hawajui kuhusu sababu walizotoa?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mara nyingi ndo wako hivyo mbona

      Delete
    2. Simba kaeka kambi Arusha na sisi tuweke kambi, Simba kafika robo fainali ligi ya mabingwa na sisi msimu huu tutafika hata kama tushatolewa kha..😀

      Delete
  2. Wanaweweseka sana viongozi wetu hasa kwenye masuala ya mipango

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic