April 23, 2014


Castle Lager kupitia ushirikiano wake na FC Barcelona leo imeanza zoezi la kusajili timu zitakazoshiriki shindano la Castle Lager Perfect 6 la mpira wa miguu litakalohusisha wachezaji sita kila upande linalofanyika kitaifa. 


Akizungumza jijini Dar es salaam jana, Meneja wa Bia ya Castle Lager, Kabula Nshimo amesema kwamba washiriki wa shindano hilo watajiandikisha kupitia bar mbalimbali nchini na kuunda timu ambazo zitashindana kupitia mabonanza yatakayofanyika maeneo mbalimbali nchini. 

“Shindano litafanyika nchi nzima ambapo timu mbalimbali katika Kanda saba zitasajiliwa na kucheza katika hatua za mtoano kwenye maeneo mbalimbali ambayo yatachaguliwa na kutangazwa mapema. Kila kanda itatoa timu moja na kufanya jumla ya timu saba ambazo zitawakilisha Kanda hizo huku timu ya nane ikitoka kwenye vyombo vya habari. Timu hizo zitachuana kwa mtoano kwenye robo fainali, nusu fainali, na hatimaye fainali.  

Nshimo alisema kwamba shindano hili limelenga kuwaburudisha wanywaji wa Castle Lager na kuwapa fursa ya kucheza soka la kujifurahisha na kufurahi pamoja. Shindano hilo litamalizika kwa kupata washindi ambao watatembelea uwanja wa Camp Nou nchini Hispania na kujionea timu ya FC Barcelona ikicheza katika ziara ambayo itagharamiwa kila kitu na Castle Lager. 

Aliongeza kuwa shindano la Perfect Six limelenga kuzungumza na wanywaji wa Castle Lager ambao wana shauku ya kucheza mpira wa miguu, kuleta pamoja wanywaji wa Castle Lager kutoka baa mbalimbali ili wafurahie pamoja, kuongeza mauzo ya Castle Lager na kuwapa zawadi wateja wa bia hiyo. 

“Pia kupitia mashindano hayo, watu sita watajishindia kiasi cha shilingi 100,000/= kupitia droo zitakazofanyika kila wiki na mwisho wa kampeni itafanyika droo kubwa ambapo watapatikana washindi wawili ambao wataambatana na na timu iliyoshinda kwenda Camp Nou Hispania”, alisema.

 Nshimo alisema kwamba timu ya waandishi wa habari itakayoshiriki fainali za kitaifa tayari imeishapatikana. “Katika kutambua mchango mkubwa wa vyombo vya habari, tukishirikiana na TASWA tulizindua shindano hili kwa kuandaa bonanza la waandishi wa habari ambao waliunda timu 8 zikashindana katika mfumo wa ligi na hatimaye timu ya Puyol ilishinda na hii ndio timu ambayo itawawakilisha wanahabari kwenye fainali za kitaifa zinazotarajiwa kufanyika Agosti mwaka huu jijini Dar es salaam. 

Nshimo pia aliwahamasisha wanywaji wa Castle Lager kwamba sasa kwakuwa tayari milango ya usajili iko wazi, watumie fursa hii vizuri kuhakikisha wanashiriki katika shindano hili la kabumbu linalotarajiwa kuleta  msisimko mkubwa kama ilivyoshuhudiwa kwenye bonanza la uzinduzi lililowahusisha wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic