MBEYA CITY WATAKUWA UGENINI MJINI MTWARA. |
Ligi Kuu Bara inatarajiwa kendelea kutimua vumbi mwishoni mwa wiki katika sita
nchini, kwa michezo minne kucheza siku ya jumamosi na michezo mwiwili kuchezwa
siku ya jumapili.
Jumamosi
uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, Kagera Sugar watakuwa wenyeji wa Simba SC
kutoka jijini Dar es salaam, huku jijini Tanga Coastal Union wakiwakaribisha
maafande wa jeshi la Magereza nchini Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa
Mkwakwani.
Ndanda FC ya
Mtwara watakuwa wenyeji wa wagonga nyundo timu ya Mbeya City katika uwanja wa
Nangwanda Sijaona, wakati maafande wa Jeshi la Kujenga Taifa Ruvu Shooting
wakicheza na ndugu zao JKT Ruvu katika uwanja wa Mabatin uliopo Mlandizi.
Siku ya
jumapili Stand United watawakaribisha wakata miwa kutoka Morogoro Mtibwa Sugar
kwenye uwanja wa Kambarage, huku Mgambo Shooting wakiwa wenyeji wa timu
ya Polisi Morogoro kwenye uwanja wa Mkwakani jijini Tanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment