July 8, 2015


Kocha mkuu wa Simba, Muingereza, Dylan Kerr, anatarajia kutumia mbinu mpya ndani ya kikosi hicho kwa kuwafanyisha wachezaji wake mazoezi matupu bila ya kugusa wala kuchezea mpira katika kambi ya timu hiyo iliyopo wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Kikosi hicho cha Simba kimeenda kujichimbia Lushoto kwa ajili ya kuweka kambi yake ya wiki mbili ya kujiandaa na michezo ya ligi kuu kwa msimu ujao.

Kerr alisema kuwa katika kambi hiyo, ameandaa programu maalumu ya kuwajenga kimwili pamoja na kuwafanya wachezaji wake kuwa na nguvu watakapopambana na wachezaji wa timu pinzani ambapo katika programu hiyo, kutakuwa hakuna kuchezea mpira hata kidogo.

“Katika kambi ya huku Lushoto, nimeandaa programu maalum ya kuwajenga na kuwafanya wachezaji wawe fiti ambapo katika mazoezi tutakayokuwa tunafanya kila siku, hatutakuwa tunagusa mpira.

“Lengo kubwa la programu hiyo ni kutaka kuwafanya wachezaji wawe imara hata pale watakapokutana na wapinzani ambao watakuwa wapo imara zaidi yetu na katika hilo, nitashirikiana na kocha wangu wa viungo, Dusan Momcilovic.


“Nimeona niwape wachezaji mazoezi hayo baada ya kuona wengi wao hawapo katika kiwango kizuri cha ‘fitness’ ambacho mchezaji yeyote yule anatakiwa kuwa nacho,” alisema Kerr ambaye aliwahi kuichezea Reading ya England.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic