July 8, 2015


Kiungo mpya wa Azam FC, Mnyarwanda, Jean  Baptiste Mugiraneza, anatarajia kutua nchini leo Jumatano na kufanyiwa vipimo kisha kufanyiwa majaribio kama ilivyo kwa kipa mpya wa timu hiyo raia wa Ivory Coast, Vincent Atchouailou de Paul Angban.

Azam tayari ina wachezaji wa kigeni watano na imebakiza nafasi mbili pekee kuweza kukamilisha wachezaji wa kimataifa saba ndani ya klabu hiyo na kwa sasa imealika wachezaji watano wa kigeni kufanya majaribio ndani ya klabu hiyo lakini mpaka sasa amewasili kipa huyo pekee.

 Ofisa habari wa timu hiyo, Jaffar Idd, alisema kwa sasa wapo kwenye maandalizi na kuangalia wachezaji wapya wa kimataifa ambao wametua klabuni hapo kwa ajili ya majaribio.

 Idd alisema kuwa, wanafanya maandalizi ya nguvu na kuangalia uwezo wa wachezaji wao kutumia michezo ya kirafiki kabla ya kuanza michuano ya Kombe la Kagame mapema wiki ijayo.

“Wachezaji wa kimataifa tumewaalika watano kwa ajili ya majaribio hapa klabuni na mpaka sasa amefika yule kipa raia wa Ivory Coast, hao wengine wataendelea kuja kuungana na timu kwa kuangalia uwezo.

“Lakini wanapotua ndani ya timu, lazima wafanye majaribio kwanza na kama tutaridhika nao ndipo tunaweza kuwapa mikataba na kocha ndiye mwenye nafasi ya kuangalia anahitaji mchezaji wa aina gani na kama ameridhika na kiwango,” alisema Idd.

Kwa upande mwingine, mmoja wa viongozi wa klabu hiyo, alisema kuwa kiungo Mnyarwanda anatarajia kutua nchini leo Jumatano.


“Mugiraneza anatarajiwa kutua leo na atafanyiwa vipimo na kuungana na wenzake kufanya majaribio kisha baada ya hapo mambo yote yatawekwa hadharani, maana mazungumzo ya awali yalishafanyika,” alisema kiongozi huyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic