July 8, 2015


Siku chache baada ya Yanga kumwongezea mkataba mshambuliaji wake raia wa Burundi, Amissi Tambwe, ameibuka na kudai kuwa thamani yake kwa sasa imeongezaka na kuwa miongoni mwa wachezaji wa bei mbaya katika kikosi hicho.


Jumamosi iliyopita, Yanga ilimuongezea mshambuliaji huyo mkataba wa mwaka mmoja na nusu wa kuendelea kubakia klabuni hapo ambapo hivi sasa ataitumikia mpaka mwaka 2017.

Tambwe alisema kuwa baada ya kupewa mkataba huo, thamani yake imeongezeka na sasa ni mmoja kati ya wachezaji wa bei mbaya katika kikosi cha timu hiyo.


Awali, wakati akijiunga na Yanga akitokea Simba, Tambwe alisajiliwa kwa dau la dola 25, 000 na mshahara wa dola 2, 000 kwa mwezi.

“Thamani yangu kwa sasa imeongezeka ukilinganisha na kipindi kile nilichojiunga na Yanga nikitokea Simba.
“Dau langu la usajili limeongezeka lakini pia mshahara nao umepanda, kwa maana hiyo naweza kusema kuwa thamani yangu imepanda na mimi ni miongoni mwa wachezaji ghali kwa kipindi hiki katika kikosi cha Yanga,” alisema Tambwe.

Alipoulizwa kuwa ni kiasi gani alichopewa na Yanga baada ya mkataba huo mpya, alisema: “ Hiyo ni siri yangu na klabu, hivyo siwezi kusema lolote juu ya hilo.”

Hata hivyo, habari za kuaminika kutoka ndani ya Yanga ambazo Championi limezipata zinadai kuwa nyota huyo amelamba dola 30,000 zaidi ya shilingi milioni 60 za usajili na atakuwa akilipwa mshahara wa dola 3,000 kwa mwezi, sawa na shilingi milioni 6.


“Uamuzi huo wa kumwongezea Tambwe mkataba pamoja na malipo hayo, ulifikiwa baada ya uongozi kutambua mchango wake wa msimu uliopita, pia baada ya kusikia kuwa anawindwa na FC Lupopo ya DR Congo na St George ya Ethiopia,” kilisema chanzo hicho cha habari.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic