July 31, 2015

JUMA ABDUL (KUSHOTO) AKIWA NA MZEE AKILIMALI...
Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, amesema kuwa kuumia kwa beki wake wa pembeni, Juma Abdul, ndiyo kumesababisha wao waondolewe kwenye michuano ya Kombe la Kagame.


Kauli hiyo aliitoa mara baada ya kumalizika kwa mechi ya robo fainali dhidi ya Azam FC, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Yanga kufungwa kwa penalti 5-3.

Juma alitolewa nje baada ya kugongwa kifuani na mshambuliaji wa Azam, Ame Ally, katika dakika ya 75 na kusababisha apoteze fahamu kabla ya Pluijm kufanya mabadiliko kwa kmuingiza, Joseph Zuttah.

Pluijm alisema kutoka kwa beki huyo kuliharibu mipango yake yote ya ushindi kwenye mechi hiyo iliyojaa upinzani.
Aliongeza kuwa, pia safu yake ya ushambuliaji ilichangia kwa kiasi kikubwa wao kutolewa kwenye hatua ya robo fainali ya Kombe la Kagame, kutokana na kushindwa kutumia nafasi nyingi.

Safu hiyo ya ushambuliaji ya Yanga iliongozwa na Mzimbabwe, Donald Ngoma, Amissi Tambwe, Geofrey Mwashiuya, Deus Kaseke kabla ya kutolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Malimi Busungu.

“Nikiri kuwa, kuumia kwa Juma kwenye mechi hii dhidi ya Azam na kusababisha ashindwe kuendelea na mechi hii kumechangia kwa kiasi kikubwa tuondolewe katika michuano ya Kagame.

“Ninaamini kuwa, kama asingeumia Juma katika mechi hii, basi matokeo yasingemalizika hivi, kufungwa kwa penalti.
“Pia, washambuliaji wangu walichangia nao tupoteze mechi hii kutokana na kushindwa kuzitumia nafasi nyingi walizokuwa wanazipata uwanjani.


“Nawapongeza viungo wangu, kiukweli walitengeneza nafasi nyingi za kufunga mabao, lakini washambuliaji Ngoma na Tambwe walishindwa kuzitumia,” alisema Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic